HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 16, 2012

KUFUNGULIWA KWA UVUVI KATIKA MTO KILOMBERO MKOANI MOROGORO

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( wa kwanza kutoka kulia ) akipinga makofi kwa pamoja na  baadhi ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo akiwemo pia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero , Ramadhan Kiombile ( wa kwanza kulia) kushangilia jambo kutoka kwa Viongozi wa Vikundi vya kupambana na kudhibiti uvuvi haramu katika Mto Kilombero ( hawapo pichani) kilichofanya kazi muda wa miezi sita tangu Desemba mosi mwaka jana hadi Juni 13, mwaka huu , wakati shughuli za uvuvi zilipofunguliwa tena na Mkuu huyo wa Mkoa.
Baadhi ya wananchi wa Mjini Ifakara, Wilaya ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro wakiangalia uteketezaji moto wa zana haramu za uvuvi zikiwemo nyavu ndogo pamoja na makokola yaliyokamatwa na Askari wa Doria wa Maliasili pamoja na vikundi vya kupambana na kudhibiti wavuvi haramu katika Mto Kilombero.


 Mkazi wa Mji wa Ifakara ambaye ni mvuvi wa samaki katika mto Kilombero, Salehe Mfuko akipanga aina ya samaki ambao wameongezeka ukubwa baada ya kusisitizwa kwa shughuli za uvuvi katika kipindi cha miezi sita kuanzia Desemba mosi mwaka jana hadi Juni 13, mwaka huu , huku wananchi wakiwaangalia sakami hao.

 Mvuvi akiongelea katika kina kirefu cha maji ya  mto Kilombero ikiwa ni  kuonesha furaha yake ya  kufunguliwa kwa shughuli za uvuvi baada ya kusitishwa kwa muda wa miezi sita kuanzia Desemba mosi mwaka jana hadi Juni 13, mwaka huu.
Mvuvi akielezea furaha yake mbele ya wananchi wa Mji huo eneo la Kivukoni kuhusu  kitendo chake cha kuongelea kwenye  kina kirefu cha maji ya  mto Kilombero ikiwa ni  kuonesha furaha yake baada ya  kufunguliwa kwa shughuli za uvuvi katika mto huo baada ya kusitishwa kwa muda wa miezi sita kuanzia Desemba mosi mwaka jana hadi Juni 13, mwaka huu. Picha zote na John Nditi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad