HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, May 23, 2012

Mbunge wa Mvomero akutana na wananchi wa kijiji cha Kinyenze kuzungumzia Mgororo wa Ardhi dhidi ya Muwekezaji wa kigeni

 Mzee Said Ahamad Kondo ( aliyesimama) akiuliza maswali  kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mbunge wa Jimbo la Mvomero , Amos Makalla ( hayupo pichani) alipokuwa katika  Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali kufuatilia mgogoro kati ya Wananchi hao na Mwekezaji wa Kizungu.
 Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makalla ( aliyesimama na kunyoosha mkono juu) akisisitiza jambo juu ya namna ya kutafuta muakafa ili  kumalizwa kwa  mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa Kitongoji cha Kinyenzi dhidi ya Mwekezaji wa kizungu.
 Ofisa Ardhi wa Wilaya ya Mvomero, Majaliwa Jafari ( aliyesimama) akitoa ufafanuzi wa  mgogoro wa shamba namba shamba 296  kati  ya wanachi wa Kitongoji cha Kinyenze na Mwekezaji wa Kizungu kwenye  mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makalla, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo , uliofanyika hivi karibini ( Mei 19) uliokuwa na lengo  la kufikia utatuzi wa mgogoro huo.
Baadhi ya wazee na wananchi wa Kitogoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera,Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, wakimsikiliza kwa makini Mbunge wa Jimbo hilo, Amos Makalla ( hayupo pichani) wakati akipowatembelea hivi karibuni ( Mei 19) wananchi wa Kitongoji hicho kwa ajili ya kupanga mkakati wa kumalizwa mgogoro kati ya mwekezaji wa kizungu na wakazi hao, Mbunge huyo pia ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo. (Picha kwa Hisani ya FATHER KIDEVU BLOG)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad