HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 11, 2011

WABUNGE WAPIGWA MSASA KUHUSU MAJUKUMU YA BOHARI KUU YA DAWA(MSD)

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya huduma za jamii Mh. Magreth Sita akitoa muongozo wa semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu majukumu ya bohari kuu ya madawa(MSD).
Mbunge wa Kawe (Chadema) Mh. Halima Mdee akiuliza swali pamoja na kutoa mchango wake kwenye semina hiyo
Baadhi ya watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na wale wa Taasisi za wizara hiyo wakisikiliza moja ya mada katika semina hiyo ya wabunge.Kushoto mstari wa kwanza ni Mganga mkuu wa Serikali Dkt. Deo Mtasiwa na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Bohari kuu ya dawa(MSD), Joseph Mgaya.
Baadhi ya Wabunge wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani, katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.Mada zilizowasilishwa ni pamoja na Muundo wa Bohari ya Dawa(MSD), Miaka 17 ya MSD;ufanisi na changamoto, Mfumo wa ugavi wa bohari ya dawa pamoja na ile ya miradi msonge.Picha na catherine Sungura-MOHSW-Dodoma

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad