

Kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha BALIMI EXTRA LAGER imetangaza rasmi ufunguzi wa mashindano ya ngoma za asili kwa mwaka huu wa 2011.
Bia ya BALIMI EXTRA LAGER imekuwa mdhamini rasmi wa mashindano haya kwa zaidi ya miaka saba sasa. Lengo kuu la kudhamini mashindano haya ni kushirikiana na wakazi wa kanda ya ziwa katika kuenzi na kulinda tamaduni za kanda alisema meneja wa bia ya Balimi Extra Lager Bi Edith Bebwa.
Vile vile ni njia moja wapo kwa wakazi kujipatia kipato cha ziada kupitia zawadi zinazotolewa na bia ya Balimi Extra Lager.
Mashindano haya yatajumuisha mikoa mitano Mwanza, Shinyanga, Tabora, Mara, Kagera na fainali kurudi tena jijini Mwanza.
Maboresho makubwa yamefanyika katika mashindano haya ya mwaka 2011 ukilinganisha na yale ya mwaka jana. Zawadi zimeongezeka mara dufu. Hii ni kuwapa changamoto wakazi wa kanda ya ziwa kushiriki zaidi kwenye mashindano haya ya ngoma za asili za mwaka 2011.


No comments:
Post a Comment