HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 30, 2010

Jeshi la polisi lawatunuku vyeti askari waliofanya vyema

Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha akimtunukia Cheo Mmoja wa wahitimu waliofanya vizuri katika mafunzo uafisa wa Polisi PC Happines Temu wakati wahitimu hao walipotunukiwa vyeti vya kumaliza mafunzo hayo leo kwenye Chuo cha maafisa wa polisi (Dar es salaam Police Academy) yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam. Wahitimu hao pia walionyesha uwezo wao wa kukabiliana na wahalifu wakati zinapotokea ghasia katika maeneo mbalimbali ya nchi na kuonyesha uwezo mkubwa katika kutumia vifaa mbalimbali ambavyo ni vya kisasa kabisa Hongera Serikali kwa kuboresha vitendea kazi kwa jeshi hilo ambalo lina kazi kubwa ya kuhakikisha raia wote wanaishi kwa amani nchini ikiwa ni pamoja na kuwaongezea mbinu mpya askari kitu kitakachowaongezea ufanisi wawapo kazini.
Mmoja wa wahitimu wa kozi hiyo ambaye pia ni mwanahabari wa Jeshi la Polisi Insp. Mohammed R. Mhina akiwa ameshikila Camera yake ya video huku akiendelea kunasa matukio mbalimbali katika mahafali hayo ya maafisa wa Jeshi la Polisi yaliyofanyika kwenye Chuo cha Dar es salaam Police Academy kilichopo Kurasini jijini Dar es salaam.
Polisi wa Kikosi Cha kuzuia Fujo FFU waliovalia mavazi ya kisasa kabisa na yenye usalama zaidi kwa askari hao wawapo kazini wakionyesha jinsi ya kukabiliana na ghasia mara zinapotokea.
Wahitimu wa mafunzo hayo wakipita kwa gwarede la Heshima mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha hayupo pichani.
Magari Maalum papya yatakayokuwa yakitumiwa na jeshi la polisi Kikosi maalum cha kutuliza fujo FFU likionyesha uwezo wake wa kuzuia ghasia kwa kurusha maji leo mbele ya wageni na waalikwa mbalimbali.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Lawrence Masha akikagua gwaride wakati wa gwaride maalum lililofanywa na wahitimu wa Chuo cha Maafisa wa Polisi Dar es salaam Police Academy kilichopo Barabara ya Kilwa Jijini Dar es salaam.
Baadi ya wahitimu wakionyesha uwezo wao wa kujihami kwa kucheza Karatee wakati walipohitimu mafunzo hayo.
Picha na mwanahabari wa Jeshi la Polisi Insp. Mohammed R. Mhina.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad