




(Picha na Executive Solutions)
MICHUANO YA KOMBE LA
TAIFA CUP YAANZA LEO
Na Ripota wetu,
Mtwara
MABINGWA wa michuano ya Kili Taifa Cup timu ya soka ya mkoa wa kisoka wa Ilala leo inashuka uwanjani kuinza safari ya kutetea ubingwa wake kwa kucheza na Mtwara katika mchezo wa ufunguzi utakao fanyika kwenye Uwanja wa Umoja mjini Mtwara.
Akizingumza jana kocha mkuu wa Ilala Jamuhuri Kiwelu alisema kuwa vijana wake wapotayari kwa mchezo huo na watahakikisha wanaendeleza rekodi yao ya kulitwaa kombe hilo kwa mara nyingi zaidi.
Katika hatua nyinge Kiwelu alisema kuwa ataianza michuano hiyo kwa kuwakosa baadhi ya wachezaji wake wa kikosi cha kwanza ambao wapo na timu ya Simba nchini Misri akiwemo mlinda lango Juma Kaseja.
Alisema wachezaji hao watajiunga na timu hiyo katika hatua ya robo fainali ambayo itafanyika jijini Dar es Salaam.
Wakati huhohuo timu ya soka ya mkoa wa Lindi nayo pia itashuka uwanjani kucheza na Ruvuma mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ilala na Mtwara.
Timu zote nne zinazochuana katika kituo cha mtwara jana zilikabidhiwa vifaa na jezi za mechi watakazocheza katika hatua ya awali.
Timu 24 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara inashiriki michuano hiyo ambayo inaanza kutimua vumbi leo katika vituo sita ikiwa ni pamoja na timu ya vijana chini ya mika 20 (Ngorongoro Heroes).
Mtwara
MABINGWA wa michuano ya Kili Taifa Cup timu ya soka ya mkoa wa kisoka wa Ilala leo inashuka uwanjani kuinza safari ya kutetea ubingwa wake kwa kucheza na Mtwara katika mchezo wa ufunguzi utakao fanyika kwenye Uwanja wa Umoja mjini Mtwara.
Akizingumza jana kocha mkuu wa Ilala Jamuhuri Kiwelu alisema kuwa vijana wake wapotayari kwa mchezo huo na watahakikisha wanaendeleza rekodi yao ya kulitwaa kombe hilo kwa mara nyingi zaidi.
Katika hatua nyinge Kiwelu alisema kuwa ataianza michuano hiyo kwa kuwakosa baadhi ya wachezaji wake wa kikosi cha kwanza ambao wapo na timu ya Simba nchini Misri akiwemo mlinda lango Juma Kaseja.
Alisema wachezaji hao watajiunga na timu hiyo katika hatua ya robo fainali ambayo itafanyika jijini Dar es Salaam.
Wakati huhohuo timu ya soka ya mkoa wa Lindi nayo pia itashuka uwanjani kucheza na Ruvuma mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ilala na Mtwara.
Timu zote nne zinazochuana katika kituo cha mtwara jana zilikabidhiwa vifaa na jezi za mechi watakazocheza katika hatua ya awali.
Timu 24 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara inashiriki michuano hiyo ambayo inaanza kutimua vumbi leo katika vituo sita ikiwa ni pamoja na timu ya vijana chini ya mika 20 (Ngorongoro Heroes).
No comments:
Post a Comment