HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 29, 2010

TBL Yatoa kitu kingine kipya,kinaitwa Grand Malt

Meneja wa TBL anaeshughulikia Bidhaa za Kimataifa,Consolata Adam akielezea namna kinywaji kipya cha Grand Malt kitakavyofanya vizuri sokoni kwani ni kinywaji kinachoweza kunywewa na mtu yeyote kutokana na kutokuwa na kilevi cha aila yeyote ile.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja akikielezea kinywaji kipya cha Grand Malt ambacho hakina kilevi kilichozinduliwa leo katika Hoteli ya City Garden,Gerezani jijini Dar.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa TBL,Nicholaus Brooks kwa pamoja wakipongezana mara baada ya uzinduzi wa kinywaji kipya cha Grand Malt uliofanyika jioni ya leo katika hoteli ya City Garden,Gerezani jijini Dar.Warembo
Wageni waalikwa wakipata kilaji laini
Wadau wa Executive Solutions,Humphrey Asamba na Carol Ndosi
Meneja wa TBL anaeshughulikia Bidhaa za Kimataifa,Consolata Adamakibadilishana mawazo na Tamika Zaun wa Executive Solutions.
wageni waalikwa.


========================


Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) leo imezindua kinywaji chake kipya cha Grand Malt ambacho hakina kilevi.


“Kinywaji hiki kipya kitaisaidia TBL kuwa na ushindani wa hali ya juu katika vinywaji vingine visivyo na kilevi kutokana na ubora na ladha yake,” alisema Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,David Minja wakati wa hafla ya uzinduzi wa kinywaji hicho katika Hoteli ya City Garden – Gerezani jijini Dar es Salaam.


Kinywaji hicho kimetengenezwa kwa maji,sukari,shayiri,lactose na vitamini huku kikiwa na ujazo wa mililita 330 katika kopo. Bei ya rejareja iliyopendekezwa na TBL ni Sh. 1,000 kwa kopo na Sh. 19,200 kwa katoni moja yenye makopo 24.


Minja alisema, Grand Malt ni kinywaji cha kipekee kutokana na ukweli kwamba kina vitamini pamoja na mchanganyiko wa maziwa.


Alisema kinywaji hicho kinawafaa wafanyakazi wenye shughuli nyingi lakini pia kinafaa kwa matumizi ya nyumbani, wafanyakazi wa usiku, wanafunzi, vikao vya kibiashara na sherehe nyinginezo.


Meneja wa TBL anayeshughulika na Bidhaa za Kimataifa,Consolata Adam alisema, “Kinywaji hiki lazima kizibe pengo la vinywaji visivyo na kilevi na bei yake inakwenda sambamba na vinywaji vingine vilivyopo sokoni.”


Alisema kinywaji hicho kimekuwa kikiuzwa katika sehemu nyingine Duniani na kutokana na hilo,TBL iliona haja ya kukizindua nchini Tanzania.

Consolata aliongeza kuwa Grand Malt ni kinywaji ambacho kinawafaa hata wanywaji wa pombe.


Kwa mujinbu wa meneja huyo, uzinduzi umeanzia Dar es Salaam na utaendelea katika mikoa mingine nchini hivi karibuni.


Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ni watengenezaji na wauzaji wa bia, vinywaji vya matunda vyenye asili ya kilevi (AFB’s) na visivyo na kilevi ndani ya Tanzania. TBL inazo hisa pia katika Tanzania Distilleries Limited na kampuni shirika, Mountainside Farms Limited.


Bia maarufu za TBL ni pamoja na Safari, Kilimanjaro, Ndovu Special Malt na Castle.

Vinywaji vingine vya TBL ni Konyagi Gin, Amarula Cream, Redds Premium Cold.

TBL imo pia katika Soko la Hisa la Dar es Salaam na imeajiri watu kiasi cha 1,300 huku ikiwa na wawakilishi katika sehemu kubwa na Tanzania na viwanda vitatu vya bia na depot nane kwa ajili ya kusambazia bia na vinywaji vingine vya kampuni hiyo.


Kwa mawasiliano zaidi


Consolata Adam

TBL, Meneja Bidhaa za Kimataifa,

+255 767 266 766

Consolata.Adam@tz.sabmiller.com


Michael Mukunza,

Executive Solutions Limited,

+255 784 978 302,

m.mukunza@executivesolutions.co.tz

mikemukunza@gmail.com


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad