HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 8, 2010

Taarifa Kwa Watanzania Waishio Canada

Kwa niaba ya Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe, naomba kuchukua fursa hii kuwajulisha kuwa Mheshimiwa Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchiniCanada kuanzia tarehe 11 Januari hadi 15 Januari, 2010.

Akiwa Ottawa Mhe. Waziri Membe atapenda kukutana na Watanzania waliokoCanada. Ubalozi unafanya utaratibu wa kupata ukumbi kwa ajili yamkutano huo ambao utafanyika siku ya tarehe 12, Januari, 2010 jionisaa Kumi na Mbili na Nusu hadi saa Tatu na Nusu usiku (6:30Pm-9:30Pm).
Tutawajulisha sehemu ya mkutano na anuwani ya shughuli hiyo kabla ya mwisho wa juma hili hivyo tunaomba muweke shughuli hii katika ratiba
zenu.

Aidha, tunaomba kila atayepata ujumbe huu atusaidie kumjulisha/
kuwajulisha Watanzania wenzetu ambao hatukuweza kuwatumia
barua pepe hii kutokana na kutokuwa na anuwani zao.

Kama mnavyojua shughuli ni watu na watu ndiyo sisi sote hivyo tunaombatujitokeze kwa wingi kuja kukutana na Mhe. Waziri Membe ambaye kama wengi mnavyokumbuka aliishi hapa Ottawa wakati akifanya kazi kwenye
Ubalozi wetu huu.

Tunawashukuru kwa ushirikiano wenu,

Kny Balozi

1 comment:

  1. Changamkeni acheni uzembe oneni wenzenu UK na USA, Abdallah Mwailubi,Calgary.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad