Na Mwandishi wetu Dar es Salaam.
Bondia
wa Tanzania Ibrahim Class anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa
mpinzani wake kutoka Mexico, Gustavo Pina katika pambano la kimataifa la
uzito wa feather litakalofanyika kesho (Septemba 30) kwenye ukumbi wa
Mlimani City.
Akizungumza
mara baada ya kupima uzito jana, Pina alisema kuwa kamwe hawezi
kupoteza mapambana mawili mfululizo na amekuja ili kurekebisha rekodi
yake baada ya kupoteza pambano la ubingwa wa WBA dhidi ya bondia kutoka
Panama, Anselmo Moreno mwezi Machi mwaka huu.
Alisema
kuwa anajua anakabiliana na upinzani mkali kutoka kwa Class, lakini
amejiandaa vilivyo kwai hawezi kurejea makosa yake tena. Kwa mujibu wa
rekodi, Class ameshinda mapambano 27 ambapo kati ya hayo, 12 kwa njia ya
KO na kupoteza mapambano sita ambapo mawili kwa njia ya KO.
Pina
ameshinda mapambano 10, matano kwa KO na kupoteza mawili yote kwa
KO.“Nimesafiri umbali mrefu kuja hapa Tanzania si kwa kushindwa, lengo
kuu ni kushinda, hivyo Class ajiandae kwani siwezi kupoteza kamwe,”
alisema Class.
Kwa
upande wake, Class alisema kuwa pamoja na kuchukua tahadhari dhidi ya
Pina, lengo lake la ushindi na kuwaomba Watanzania kufika kwa wingi.
“Ushindi wangu wa KO upo pale pale na si vinginevyo.
Nimejiandaa
vyema kwa ajili ya kuwapa heshima Watanzania na si vinginevyo,” alisema
Class.Pambano hilo limeandaliwa na kampuni ya MO Boxing, ikiwa ni mara
ya kwanza kwa kampuni hiyo chini ya mfanyabiashara maarufu, Mohammed
Dewji.
Mratibu
wa pambano hilo kutoka MO Promotion Ahmed Seddiqi alisema kuwa
maandalizi yamekamilika na ambapo kutakuwa na mapambano sita ya
utangulizi.
Pambano
la kwanza la utangulizi litakuwa kati ya bondia nyota wa Ghana, Alfred
Lamptey ambaye atapambana na bondia Abraham Ndauendapo kutoka Namibia
huku Juma Choki akizichapa na bondia wa kutoka Mexico Jose Hernandez
ambapo bondia kutoka Kenya Nicholas Mwangi atapimana ubavu na Emmanuel
Mwakyembe wa Tanzania.
Pambano
lingine litakuwa baina ya bondia Sameer Anwar dhidi ya Adam Mrisho huku
Mwinyi Mzengelaakizichapana Sabari J na pambano lingine litakuwa baina
ya Lulu Kayage dhidi ya Sadra Mohamed.
Pambano hayo yamedhaminiwa na kampuni ya Azam TV, Boxer, MO XTRA, Mlimani City, KCB Bank, White Sands Resorts, Bajaj na OTAPP.
Bondia
Ibrahim Class (Katikati) akipima uzito kuelekea pambano la kesho dhidi
ya mpinzani wake kutoka Mexico, Gustavo Pina (wa tatu kulia).
Mabondia
Juma Choki (Tanzania) na mpinzani wake kutoka Mexico, Jose Hernandez
wakitunishiana ubavundia wa kike Lulu Kayage dhidi ya Sadra Mohamed.
Mabondia wa kike Lulu Kayage (kulia) na Sadra Mohamed wakitambiana kabla ya pambano lao la kesho.
No comments:
Post a Comment