HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 17, 2022

Rais Samia afungua Barabara ya Nyahua-Chaya km 85.4 Mkoani Tabora

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed SH. Albahar wakizindua rasmi barabara ya Nyahua-Chaya 85.4 km kwenye Sherehe za ufunguzi wa barabara hiyo katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022. Wengine katika picha ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani, pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Rogatus MativilaRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed SH. Albahar, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila, akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Barabara ya Nyahua-Chaya yenye 85.4 km katika Sherehe zilizofanyika Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED) Waleed S. Albahar wakati akiwapungia mkono wananchi waliojipanga kando ya barabara ya Nyahua-Chaya mara baada ya ufunguzi uliofanyika katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Nyahua-Chaya yenye 85.4 km zilizofanyika Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei,2022.


Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia katika Sherehe za ufunguzi wa barabara ya Nyahua-Chaya 85.4 km zilizofanyika katika Kijiji cha Tura, Uyui mkoani Tabora tarehe 17 Mei, 2022.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad