Mkurugenzi
wa Tanzanian Men As Equal Partiners in Delvelomepment(TMEPiD)
Dkt.Cuthbert Maendaenda akizungumza na waandishi wa habari na Wahariri
kuhusiana Masoko Jumuishi ya Uzazi wa Mpango mara baada ya kuwajengea
uwezo katika Mkutano uliofanyika Morogoro.
Meneja wa Utetezi wa Shirika la Tanzania Communication and Development Centre (TCDC), James Mlali akizungumza na waandishi habari kuhusiana uzazi wa mpango katika semina iliyoandaliwa na TMEPiD kwa ufadhili wa UNFPA iliyofanyika mkoani Morogoro.
Baadhi ya Wahariri na Waandishi wa Habari wakiwa katika mkutano.
Picha ya pamoja ya waandishi wa habari na wahariri mara baada ya kupata mafunzo ya juu hali ya uzazi wa mpango nchini.
Meneja wa Utetezi wa Shirika la Tanzania Communication and Development Centre (TCDC), James Mlali akizungumza na waandishi habari kuhusiana uzazi wa mpango katika semina iliyoandaliwa na TMEPiD kwa ufadhili wa UNFPA iliyofanyika mkoani Morogoro.
Baadhi ya Wahariri na Waandishi wa Habari wakiwa katika mkutano.
Picha ya pamoja ya waandishi wa habari na wahariri mara baada ya kupata mafunzo ya juu hali ya uzazi wa mpango nchini.
*Tafiti zinaonyesha uzazi wa mpango ukitumika vizuri vifo vya mama na mtoto vitapungua.
*TMEPiD yaja na ushauri wa masoko jumuishi ya upatikanaji wa huduma za uzazi wa mpango.
Na Chalila Kibuda ,Michuzi TV
IDADI
ya watu kuwa kubwa sio kigezo cha kuwa na maendeleo kwani baadhi ya
nchi zimekuwa na idadi ndogo za watu lakini hazijaweza kupata maendeleo .
Suala
la uzazi wa mpango haliko kwa ajili ya kufanya idadi ya watu kuwa
ndogo bali ni kufanya kuwepo kwa idadi ambayo serikali inaweza kupanga
bajeti pamoja na kuwa na idadi kubwa ya watu wenaozalisha huku idadi
ndogo ikiwa tegemezi.
Uzazi
wa mpango ni hiari ya mtu kuamua muda gani wa kuweza kupata mtoto na
mtu huyo kuamua ni mtu gani wa kuamua kupata naye mtoto kwa ajili ya
kuweza mtoto huo kupata huduma zote katika ukuaji na kulinda afya ya
mama.
Meneja
wa Utetezi wa Shirika la Tanzania Communication and Development Centre
(TCDC), James Mlali anasema huduma za uzazi wa mpango ni muhimu zaidi
katika kuboresha afya ya mama, afya ya mtoto ikiwemo kuleta maendeleo
kwa ujumla kwa kusaidia serikali kupanga bajeti ambayo inaweza
kutusheleza.
Meneja
wa Utetezi wa Shirika la Tanzania Communication and Development Centre
(TCDC), James Mlali akizungumza na waandishi habari kuhusiana uzazi wa
mpango katika semina iliyoandaliwa na TMEPiD kwa ufadhili wa UNFPA
iliyofanyika mkoani Morogoro
Mlali
anasema, umuhimu huo, juhudi zinapaswa kufanywa ili kuongeza huduma
hizo nchini kuanzia maeneo yote ya vijijini na mijini pamoja na kuruhusu
sekta binafsi kushiriki katika kutoa huduma jumuishi ya soko la huduma
za mpango.
Mlali
aliyasema hayo katika Semina juu ya Mbinu Jumuishi za Soko la Huduma
za Uzazi wa Mpango zinazoweza kupatikana kiurahisi kwa kila anayehitaji
na kuwa endelevu kuliko ilivyo sasa.
Semina
hiyo ya Desemba 14 hadi 16, 2021 ambayo iliwakutanisha pamoja wahariri
wa vyombo mbalimbali vya habari nchini ilifanyika mjini Morogoro ambapo
iliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali ambalo limejikita katika
kukuza ushiriki wa wanaume katika Afya na Haki za Ujinsia na Uzazi ,
afya ya mama na mtoto pamoja na kukuza usawa wa kijinsia katika shughuli
za maendeleo ya kijamii na kiuchumi la Tanzania Men as Equal Partners
in Development (TMEPiD) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa
Linaloshugulikia Idadi ya Watu (UNFPA) pamoja na wengine katika utetezi
wa uzazi afua za uzazi wa mpango nchini.
Amesema
huduma za uzazi wa mpango nchini bado kuna haja ya kufanya kazi
zaidi,ili tuweze kupiga hatua, kulingana na taarifa rasmi za afya na
idadi ya watu za mwaka 2015 hadi 2016 ya Tanzania Demographic and Health
Survey, tunaona kuwa watumiaji wa huduma za uzazi wa mpango walifikia
asilimia 32 katika kila asilimia 100, ambacho ni kiwango kidogo,
hawajafikia hata theluthi.
Amesema
matumizi ya kila mwaka zinaonyesha kuwa, kufikia mwaka 2020 idadi hiyo
ilikuwa imefikia asilimia 41 ambapo malengo yake ni kuhakikisha
watumiaji hao wanafikia asilimia 47 mwaka 2023.
Amesema
kuweza kufikia asilimia 47 jitihada zinahitajika kwa serikali kufanya
zaidi kwa kushirikisha wadau kufanya kazi zaidi ili watumiaji wa
huduma za uzazi wa mpango waweze kuongezeka nchini ikiwa pamoja na
kusogeza huduma kila sehemu ambapo huduma hizo zinaweza kukaa ikiwemo
Famasi na Maduka ya Dawa Muhimu kama iliyo kwa kwa huduma za Kondomu.
"Lengo
sio kuwa na idadi kubwa ya watumiaji, bali ni kufanya kuongezeka kwa
huduma za uzazi wa mpango kurahisisha watu kuzifikia na kuweza kutoa
mchango mkubwa sana katika afya ya mama, afya ya mtoto na maendeleo kwa
ujumla,"amesema Mlali.
Amesema
kuwa kutokana na huduma hizo kupatikana kidogo karibu ya mimba zote
zinazotungwa baadhi ya mimba ambazo hazikutarajiwa kuwa wanapanga kuwa
wazae, wengine wana mtoto mdogo, wengine umri umeenda sana, hana malengo
ya kuzaa, lakini baada ya kushiriki tendo wanajikuta wamepata mtoto.
"Tafiti
Ulimwengunj zinaonyesha kuwa matumizi ya huduma za uzazi wa mpango
zikifanyika vizuri, vifo vya akina mama vinavyotokana na uzazi vinaweza
kupungua kwa asilimia 44,na vifo vya watoto vinaweza kupungua kwa
asilimia 35.
"Taifa
linahitaji nguvu kazi kubwa, linahitaji wanawake wenye afya njema,
linahitaji watoto wakue vizuri, wasikatishwe au maisha yao yasikatishwe,
katika umri mdogo waweze kukuwa ili waweze kuwa sehemu ya nguvu kazi ya
Taifa.
Amesema
huduma za uzazi wa mpango zina mchango mkubwa katika maendeleo kwa
sababu ndizo ambazo zinasaidia familia, au watu binafsi kuamua idadi ya
watoto ambao wanataka kuzaa, wawazae kwa wakati gani, wawaachanishe kwa
umri gani kati ya mtoto na mtoto na hizo ndiyo kanuni bora kwa ajili ya
afya mama na mtoto kwa maendeleo ya nchi.
Mlali
anasema kuwa, Serikali inapaswa kuelekeza bajeti ya kutosha kwenye
masuala yahusuyo uzazi wa mpango na inapaswa kupewa kipaumbele kikubwa,
pia jamii ambazo zina fikira potofu kuhusu uzazi wa mpango zinapaswa
kuachana nazo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa TMEPiD, Dkt.Cuthbert Maendaenda katika semina
hiyo amesema kuwa, kila mtu ana haki ya kuamua ni wakati gani wa kuzaa
na wakati gani si wa kuzaa kutokana mipango katika familia.
Amesema
taasisi yaob inahusika na utetezi na kuimarisha elimu afya ya uzazi
katika jamii hasa ikiwalenga wanaume, kwa nini tunawalenga wanaume? Kwa
sababu mbalimbali za kijamii, walikuwa ni kundi ambalo limewekwa pembeni
katika masuala ya haki ya uzazi pamoja na uzazi wa mpango
"Ukitamka
sema uzazi wa mpango moja kwa moja zinawalenga wanawake, njia za uzazi
wa mpango nyingi zinawalenga wanawake, huduma zinazotolewa mahali
zinawalenga mama na mtoto, hivyo wanaume walikuwa wanakaa
pembeni.Tukiangalia kimila, wanaume ndiyo wafanya maamuzi,kama ni mzazi
mtoto apatikane lini, wapatikane watoto wangapi, maamuzi mara nyingi
yanategemea wanaume, mila zimewapa hiyo nguvu au upendeleo.
"Kwa
hiyo, kwa sasa Taasisi tumejikita katika kujiimarisha kwenye utetezi wa
afya ya uzazi wa mpango, tukisaidiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la
Idadi ya Watu hapa Tanzania (UNFPA)na kwa sababu tayari Serikali
imeshajiwekea malengo, Malengo ya Uzazi wa Mpango 2030, Serikali
imepania kupanua matumizi ya huduma za uzazi wa mpango.
Dk.Maendaenda
amesema kupanua wigo wa wananchi kuweza kupata huduma za uzazi wa
mpango, sasa katika kufanya hivyo, tukajikuta miaka mingi mtu akitaka
kupata huduma ya uzazi wa mpango alipaswa kwenda kiliniki, usipokwenda
kiliniki hauwezi kupata huduma,lakini pia kuna watu wengine wanapata
changamoto ya kupata huduma, ukienda kiliniki au zahanati huduma hamna,
kwenye jamii zingine ambapo vijana ambao ndiyo wapo kwa wingi zaidi,
suala la uhusiano wamekuwa wakishindwa kufikia hizo huduma kwa sababu ya
hofu ya wazazi wao, ndugu zao kuwa wanaweza kukutana nao na kuaza
kuhojiana juu ya kilichowapeleka .
"Tumekuja
na masoko jumuishi (TMA) katika hili tunachotaka ni huduma ya uzazi wa
mpango zipatikane kila mahali, na kupitia wadau si kwenda kliniki,
tukiangalia huko miaka ya nyuma hata kupata huduma ya baba, mpira wa
kiume au kondomu ilikuwa lazima uende kliniki, lakini kwa sasa ukitaka
kondomu inapatikana kila mahali ikiwemo katika maduka ya rejareja.
"Mtu
hawezi kuacha kutumia kondomu, kwa sababu inapatikana kila mahali, na
kwa sababu tunataka huduma nyingine zipatikane kila mahali za uzazi wa
mpango ikiwemo katika famasi na maeneo mengine ili ziweze kupatikana kwa
wingi hususani mashirika yanayotoa huduma hizo. Kwa hiyo mtu hawezi
kuacha kutumia kondomu,"amesema Dkt.Maendaenda.
Amesema
Taifa litapata faida nyingi kupitia upangaji salama wa uzazi wa mpango
na hakutakuwa na kisingizio cha mtu kushindwa kuitumia huduma hiyo
kutokana na kuweza mazingira mazuri ya huduma hizo.
"Tunataka
huduma za uzazi wa mpango zipatikane kila mahali wakati wowote, kwa
mfano katika maduka ya kutolea huduma za dawa kwa kuwapa
mafunzo,mashirika kama TMARK,PSI ambao wapo mitaani, kwa hiyo, mwanamke
au mwanaume akitaka huduma asilazimishwe, kama tumeweza kuzileta kondomu
zikajaa, basi itafutwe njia nyingine ya kuhakikisha huduma zingine za
uzazi wa mpango zinasambaa kila mahali.
Aidha
amesema kuwa, idadi kubwa ya watu wanaoishi mijini wana uwezo hivyo
inawezekana wakawa wanapatiwa huduma hizo kwa kugharamia ili kipato
kitakachopatikana kiweze kupeleka huduma hiyo kwa wingi huko vijijini.
"Hii
ni faida kubwa ya kuhakikisha maeneo ya vijijini huduma zinajaa,
lakini pia tunatetea kwamba haya mashirika ya Bima na wenyewe katika
huduma wanazotoa waweke suala la uzazi wa mpango ili kama huduma hiyo
inatolewa katika vituo binafsi, waweze kufanya maamuzi ya kwenda kutumia
huduma anapotaka,
"Pia
itaweza kusaidia kuongeza usiri, kwa mtu ambaye anataka huduma
hiyo,anaweza kuipata sehemu yoyote bila kukaa foleni,kwa hiyo unajua
mimi ninatumia huduma fulani unaenda kwenye duka la dawa kupata huduma,
hivyo kama mwingine anatumia kitanzi badala ya kwenda kliniki na
kuambiwa kuwa havipo, ataweza kwenda kununua na kuja kuwekewa katika
kituo cha afya.
"Pia
itatoa nafasi kwa watumiaji wa huduma ya uzazi wa mpango mfano wanaume
kupata nafasi ya kukaa na wahudumu kupata ushauri kabla ya kufanya
maamuzi,"amesema.
Dkt.Maendaenda
amesema kuwa, pia elimu kuhusu huduma za uzazi wa mpango iendelee
kutolewa katika maeneo yote nchini ili kupunguza changamoto kwa baadhi
ya makundi hususani vijana.
Amebainisha
sasa huduma za uzazi wa mpango ni bure na zinatolewa na Serikali,
lakini wakati mwingine bajeti ya Serikali inakuwa haitoshelezi soko la
wahitaji.
Amesema
tafiti zinaonesha kuwa, kuna njia nyingi za uzazi wa mpango ambazo
zinaweza kutumiwa na mtu au wenza waweze kusubiri,kuchelewesha au
kupunguza idadi ya watoto watakaowazaa. Miongoni mwa njia hizo kuna njia
za muda mfupi, muda mrefu na za kudumu.
Amesema njia za kisasa za uzazi wa mpango ambazo unaweza kuzibadilisha, unaweza kupata ujauzito pindi utakapoacha kuzitumia.
Wataalamu
wa afya wanaeleza kuwa, njia hizi ni nzuri kwa mama anayetaka kupata
ujauzito baada ya miaka miwili baada ya kujifungua na miongoni mwa njia
hizo ni vichecheo ambavyo ni sawa na vichocheo vya kawaida
vilivyomo kwenye mwili wa mwanamke, njia ya vidonge ambavyo hutumiwa na wanawake kila siku.
Njia
ya nyingine ni ya sindano ambapo mama huchoma sindano kila baada ya
miezi mitatu,njia ya dharura ya vidonge vya uzazi wa mpango ambavyo huwa
vinamezwa na mama ili kuzuia kupata mimba kwa mama anayeshiriki tendo
la ndoa au ngono bila kutumia kinga yeyote.
Hivi
vinaweza kuzuia mimba hadi siku tano baada ya kujamiana, kondomu za
kike na kiume nazo ni muhimu kutumia ipasavyo kila unapofanya tendo la
ndoa au ngono. Hii ni njia ya pekee ambayo pia inazuia maambukizi ya VVU
na magonjwa ya zinaa.
Dk.Maendaenda
inawezekana ikiwa mama anaufahamu mzunguko mzima wa siku zake za hedhi
na kujua ni zipi siku za hatari za kushika mimba hiyi mama na mwenza
wake wanatakiwa kuacha kabisa kufanya tendo la ndoa au ngono siku hizo
za hatari.
Pia
kufunga kizazi kwa mwanaume ambapo njia hii inahusisha upasuaji mdogo
ambapo mirija ya uzazi ya mwanaume ukatwa au kufungwa hivyo kuzuia yai
kusafiri na kukutana na shahawa ambapo licha ya kufanya hivyo mwanaume
anaendelea kuwa na hamu ya kujamiiana na kutoa mbegu, lakini mbegu zake
hazitaweza kutunga mimba.
Kufunga
kizazi kwa mwanamke ni njia inahusisha upasuaji mdogo inafanyika kwa
kuziba au kukata mirija ya kizazi kuzuia yai kukutana na mbegu, mwanamke
ataendelea kuwa na hamu ya kujamiiana na kuona siku zake za hedhi.
No comments:
Post a Comment