Na Marco Maduhu Shinyanga. 
Shirika
 la Investment in Children and their Societies (ICS) limeungana na 
Serikali mkoani Shinyanga kuzindua mpango mkakati wa kutokomeza matukio 
ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, ambao utadumu kwa muda wa miaka 
mitano, ili kusiwepo tena na matukio hayo mkoani humo zikiwemo mimba na 
ndoa za utotoni.
Mpango
 huo umezinduliwa jana katika Kata ya Segese halmashauri ya Msalala 
wilayani Kahama, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani 
Shinyanga, likiwamo Shirika la ICS, AGAPE, Rafiki SDO, WFT,Mtandao wa 
Kijinsia Tanzania TGNP, UN WOMEN, UNFPA na KOICA.
Akizungumza
 wakati wa uzinduzi wa mpango huo, Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab 
Telack, amesema Serikali ya mkoa huo ni ya kwanza hapa nchini kati ya 
mikoa 26 , kuzindua mpango wake mkakati wa kutokomeza matukio ya ukatili
 dhidi ya wanawake na watoto. 
“Tumezindua
 mpango huu mkakati  wa kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake 
na watoto, ambao utadumu kwa muda wa miaka mitano, kuanzia (2020-2025) 
kwa kuonyesha dira ya mkoa, na kubainisha changamoto zilizopo katika 
mkoa wetu ambazo ni chanzo cha matukio haya na kuzifanyia kazi,”amesema 
Telack. 
“Mashirika
 yote yasiyo ya kiserikali katika utekelezaji wao wa miradi ya mpango 
mkakati wa kitaifa wa Serikali wa kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya
 wanawake na watoto MTAKUWWA, watautumia mpango huu ambao tumeuzindua 
leo na kuwa kama dira yao,”ameongeza. 
Aidha
 amesema kazi  ya kuandaa mpango huo umefanywa na viongozi wa Serikali 
mkoani Shinyanga, kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo mkoani humo, 
likiwamo Shirika la ICS, Women Fund Tanzania (WFT) ,Rafiki SDO, pamoja 
na AGAPE, ambapo pia wameshiriki kufadhili uzalishaji wa nyaraka za 
vitabu na uzinduzi wa kitabu hicho cha mpango mkakati. 
Ameitaka
 jamii ya mkoa wa Shinyanga, kuachana na matukio ya ukatili dhidi ya 
wanawake na watoto, pamoja na kuacha kuendekeza mila potofu  ambazo ni 
kandamizi zilizopitwa na wakati. 
Amesema
 dhamira ya mkoa huo ni kuona kunakuwepo na usawa wa kijinsia kwenye 
nyanja zote, zikiwemo shughuli za kiuchumi, pamoja na watoto wa kike 
kuwa sawa kimasomo na wa kiume, na kuacha tabia ya kuwaozesha ndoa za 
utotoni na  kuzima ndoto zao. 
Naye
 Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, 
Wazee na Watoto, Sifuni Msangi, ameipongeza Serikali ya mkoa wa 
Shinyanga, kwa kuzindua mpango wake mkakati wa kutokomeza matukio ya 
ukatili dhidi ya wanawake na watoto, ambao ni moja ya utekelezaji wa 
MTAKUWWA, ambao umelenga ifikapo mwaka 2025 matukio hayo ya ukatili yawe
 yamepungua. 
Kwa
 upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Investment in Children and their 
Societies (ICS) Kudely Sokoine, ambao ni miongoni mwa wadau wakubwa 
walioshiriki  kuandaa mpango mkakati  wa mkoani Shinyanga wa kutokomeza 
matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, amesema wao wataendelea 
kuutumia mpango huo katika kutekeleza miradi yao ambayo tayari shughuli 
hizo wanazifanya ndani ya jamii. 
Amesema
 ili kuwa na Taifa zuri, lazima kuwepo na usawa wa kijinsia, na ndio 
maana Shirika hilo limekuwa mstari wa mbele kwa kushirikiana na Serikali
 pamoja na mashirika mengine, kupambana kutokomeza matukio hayo ya 
ukatili ndani ya jamii dhidi ya wanawake na watoto. 
TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akizungumza kwenye uzinduzi wa 
kitabu cha mpango mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza 
matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Katibu
 tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, akizungumza kwenye uzinduzi
 wa mpango mkakati wa Serikali mkoani humo wa kutokomeza matukio ya 
ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akimkabidhi kitabu cha mpango huo 
mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza matukio ya ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto, Mkurugenzi mkazi kutoka shirika la umoja wa
 mataifa na idadi ya watu (UNFPA) Dr. Willfred Ochani. Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akimkabidhi kitabu cha mpango huo 
mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza matukio ya ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto, Mkurugenzi mkazi kutoka Shirika la 
maendeleo la korea Koica Kyucheol Eo.
Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akimkabidhi kitabu cha mpango huo 
mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza matukio ya ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto, Mkurugenzi mkazi kutoka Shirika la 
maendeleo la korea Koica Kyucheol Eo. Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akimkabidhi kitabu cha mpango huo 
mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza matukio ya ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto, Makamu mwakilishi wa mashirika 
yanayojihusisha na usawa wa kijinsia (UN WOMEN) Julia Broussard.
Mkuu
 wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, akimkabidhi kitabu cha mpango huo 
mkakati wa Serikali mkoani Shinyanga wa kutokomeza matukio ya ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto, Makamu mwakilishi wa mashirika 
yanayojihusisha na usawa wa kijinsia (UN WOMEN) Julia Broussard.
Awali
 mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Zainab Telack, akiingia uwanjani tayari kwa 
kuzindua kitabu cha mpango huo mkakati, akiwa na mkuu wa wilaya ya 
Shinyanga Jasinta Mboneko, pamoja na mkuu wa wilaya ya Kshapu Nyabaganga
 Taraba.
Na Marco Maduhu- Shinyanga.
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment