Charles James, Michuzi TV
CHUO
 cha Uhasibu Arusha (The Instistute of Accontancy Arusha IAA) ambacho 
kipo chini ya Serikali  kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kinatarajia  
kufungua tawi (Campas) la Chuo hicho katika Mkoa wa Dodoma lengo likiwa 
 kuunga Mkoano Jitihada za Serikali katika Sekta ya Elimu .
Akizungumza
 leo na wandishi wa habari jijini Dodoma Mkuu wa Chuo hicho Profesa 
Eliamini Sedokeya amesema ili kuweza kuendana na jitihada za serikali 
wameona ni vyema kama chuo wakatoa mchango wao katika kuhakikisha kwamba
 wanaongeza tawi (Campas).
‘’ Kuzingatia kuwa nchi imehamia 
katika Makao Makuu ya nchi yamehamia Dodoma kwahiyo sisi kama chuo 
tukasema na sisi ni wajibu na niwakati muafaka wa sisi kwenda Dodoma ‘’
Amesema
 toka awamu ya tano ilivyoingia madarakani kumekuwa na mabadiliko 
makubwa katika sekta ya Elimu kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania Dkt Jonh Pombe Magfuli alikuja na mpango wa kutoa Elimu bure 
kwamaana ya Elimu bila malipo katika ngazi za msingi na sekondari hivyo 
hiyo imepelekea mahitaji katika vyuo kuongezeka sana
‘’ kwahiyo 
unaona ongezeko hilo wote labda hawataweza kwenda high school lakini 
vile vile wakija vyuoni masalani inawezekana tusiweze kuwapokea wote 
kwahiyo ili kuendana na jitihada za serikali tukaona kama chuo tutoe  
mchango wetu kuhakikisha kwamba tunakua.’’
Profesa Sedoyeke 
amesema mpaka sasa wametafuta katika la eneo Njendengwa wamelilipia 
ambapo kwa sasa wapo katika hatua za mwisho kwaajili ya kupata hati  na 
tayari michoro na taratibu nyingine za ndani za kibali kwaajili ya 
kuanza kujenga zimekwisha kuanza.
‘’ Kwa hiyo sasahivi kufungua 
tawi (Campas) Dodoma ni kitu ambacho kipo tayari kwenye mwendo na 
tunategemea mwakani tukawa na tawi (Campas) ambayo iko kamili inayotoa 
kozi zote kuanzia ngazi ya cheti mpaka Masters’’ Amesema Prof Sedoyeke.
Amesema
 mpaka sasa wanakozi hamsini (50) huku wakijiendesha katika Matawi 
makubwa matatu  ikiwemo Arusha,Babati na Dar es salaam.
‘’mpaka 
sasa tunawanafunzi takribani elfu tano tukiwa na waajiriwa kama mia 
mbili ishirini vile vile chuo kimeendelea kushirikiana na taasisi  
mbalimali kama jeshi ,"
Chuo cha uhasibu Arusha ni chuo cha 
Serikali kilicho anzishwa miaka ya themanini kama kituo cha kutengeneza 
wataalamu wa uhasibu baada ya hapo serikali iliona umuhimu wa kuwa chuo 
kamili ,sheria ya Namba moja (1) 1990 ikaanzisha chuo rasmi ambapo kwa 
sasa wanakwenda miaka thelathini ya chuo hicho . 
Mkuu
 wa Chuo cha Uhasibu Arusha IAA akifafanua jambo kwa wandishi wa habari 
jijini Dodoma alipokua akitangaza azma ya Chuo hicho kufungua tawi lake 
jijini Dodoma ukiwa ni mpango wao wa kuunga mkono juhudi za serikali 
kuhamia Makao Makuu ya Nchi jijini Dodoma. 
 

 
 

 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment