HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 1, 2019

Miezi 15 ya mradi wa elimu kwa vishikwambi wakamilika

SERIKALI imetaka watoto wote walioshiriki katika mradi wa XPRIZE-Unesco wa kujua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu kwa kutumia Vishikwambi katika mradi wa majaribio mkoa wa Tanga kuhakikishwa wanaendelea na elimu katika shule shirikishi za mkoa huo.

Mradi huo wa XPRIZE umekamilisha awamu yake ya miezi 15 na mafanikio yake ni makubwa.

Akizungumza mjini Korogwe wakati wa kufunga mradi huo, Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said alisema kwamba mradi huo ulilenga kupeleka elimu kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu unastahili kuingia awamu ya pili kabla ya mafanikio yake kusambazwa nchi nzima.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bi. Zena alisema kwamba kwa sasa wanafanya mchakato wa kuwa na awamu ya pili ya mradi huo ambao utaondoa changamoto zilizopo kabla ya kusambazwa nchini kote.

Mradi huo ulioanza Desemba 2017 umefikia mwisho wake Aprili mwaka huu na umeelezwa kuwezesha watoto walioshiriki kufanya vyema katika masomo hayo waliojifunza bila Mwalimu kwa kutumia michezo iliyopo kwenye Vishikwambi.

Watoto wanaohusika ni wa miaka 5 mpaka 12. Imeelezwa kuwa kwa matumizi hayo ya Vishikwambi na mafanikio yake inaonesha kuwa njia nyingine ya kurejesha watoto wengi waliokosa elimu, darasani kwa kutumia teknolojia upo sahihi.

Bi. Zena alisema hakuna shaka kwamba elimu ni muhimu na kutokana na ukweli huo, mradi umedhirisha uwezo wake wa kusaidia wasioipata kwa kawaida kuipata. Katika kuimarisha kwenye mchakato wa pili kwa kuangalia matatizo yaliyopunguza kasi, serikali inaona Vishikwambi vibaki shule kwa usalama na pia walimu kutumika kuwezesha watoto wengi zaidi kujua kwa kasi KKK huku wakiimarisha uwezo wao wa kutumia teknolojia kujilete maendeleo.

Alisema pamoja na kunufaisha watoto mradi huo pia umefanikiwa kisaikolojia kushawishi watoto zaidi kupenda kusoma na kuanza mapema kutengeneza uongozi hasa kwa vijana ambao kutokana na kujua kusoma wamekuwa maarufu katika vijiji vyao.

Alitaka pamoja na kumalizika kwa mradi huo, wasimamizi wa sola katika vitongoji 170 kuhakikisha kwamba wanatunza sola hizo ili kusaidia vijana hao na watu wengine kufanyia kuchaji.

Mafanikio ya mradi huo kunaongeza nafasi zaidi kwa mujibu wa sera ya serikali ya kuhakikisha kwamba watoto wote hata wale ambao hawakuingia katika mfumo rasmi wanaingiza katika mfumo wa elimu kwa kupitia taratibu mbalimbali. Kwa sasa taratibu hizo ni utaratibu wa Memkwa kwa elimu ya msingi na Mespa kwa sekondari

Mradi huo ambao umefungwa ni sehemu ya mradi wa majaribio wa dunia ambapo teknolojia inajaribiwa kusaidia wale waliokosa nafasi ya kuingia shule.

Wakati mradi huo unaanza mwakilishi wa Global Learning Xprize, Elianne Philibert  alisema kwamba mafanikio yake yatawezeshwa kutengenezwa kwa moduli za kufundishia watoto walio nje ya mfumo rasmi wanaotumia lugha ya Kiswahili.

Washiriki wa mradi huo wa XPRIZE chini ya uangalizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) na Kamati ya kitaifa inayohusisha pia Wizara ya Elimu imelenga kuwapata watoto ambao wanaweza kuingizwa darasa la pili na kuendelea na pia kuongeza uwezo wa kumudu masomo kwa watoto wa darasa la pili. Mradi huo ni matokeo ya mashindano Global Learning XPRIZE yaliyozinduliwa na Taasisi ya XPRIZE Septemba 2014.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos alisema katika hafla hiyo kwamba mradi huo  ulisohirikisha wilaya sita za Handeni, Korogwe, Lushoto, Mkinga, Muheza, na Pangani umekuwa na mafanikio kutokana na kujitoa kwa wadau wa mradi huo na wale ambao wamepelekewa.

Alishukuru serikali ya Tanzania kwua kushiriki katika shindano na pia kutekeleza malengo ya mradi huo. Alisema mradi huo ni utekelezaji wa wazo la UNESCO kwamba elimu ni tumaini jema  lakufikia maendeleo.

“Mradi wa XPRIZE umedhirisha kwamba mafunzo au utoaji elimu kwa watu ambao wamekosa au wana mazingira magumu unaweza kuboreshwa kwa ubunifu wa watoto kujifunza wenyewe kwa kutumia mifumo ya komyuta kama ilivyokuwa kwa vishikwambi “ alisema Tirso.

Alisema kabla ya mradi huo washiriki wake asilimia 74 walikuw ahawajwahi kugusa jingo inaloitwa shule, asilimia 80 walikuwa wanajifunza nyumbani na asiimia 90 walikuwahawawezi kusoma hata neon moja la Kiswahili ambalo ni lugha yataifa.

“Baada ya miezi 15  namba hizo zimepunguzwa kwa zaidi ya nusu huku watoto hao wakijifunza takribani sawa na watu walioshiriki darasani kwa kipindi cha mwaka mzima” alisema.

Kutokana na mafanikio hayo UNESCO imeitaka Wizara ya Elimu kusambaza zaidi wazo la mradi huo ili kuwafikia watoto wengi zaidi waliopemnbezoni na mazingira magumu yamaisha.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais Tamisemi ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli, Bi Odilia Mushi alisema kwamba mradi huo umefanikiwa na kwamba nia ya serikali kuuimarisha na kuutambua zaidi kabla ya kuutawanya nchini.

Alisema pamoja na kuibua hamasa, ushuhuda wa watoto wenyewe unaonesha kwamba teknolojia inaweza kutumika kufungua maeneo yenye matatizo ya kufikika.

Aidha Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu akimkaribisha mgeni rasmi alisema kwamba watoto ambao walikuwa wamekosa elimu wamepata faida kubwa ya mradi huo hasa wa kujua kuandika kusoma na kuhesabu.

“Hawawezi kuandika kwa kutumia kalamu lakini wanaweza kuandika kwa kutumia Vishikwambi na ni hatua kubwa ya kujua teknolojia na matumizi yake” alisema.

Mmoja wa wazazi Stella Ernest, aliishukuru serikali ya awamu ya Tano kwa kuwezesha kuwapo kwa programu hiyo ambayo imewatoa kimasomaso. Alisema watoto wamekuwa werevu zaidi na kutambua mambo katika hali ya kisasa kuliko awali.

Alisema hata mtoto wake mdogo siku hizi kwa kufurahishwa na michezo iliyopo katika Vishkwambi hivyo anapoamka humuuliza mama yake kama anajua kuandika Ameitaka serikali kuboresha zaidi mradi huo na kuufanya kuwa endelevu ili kusaidia watoto wengi zaidi. Aidha alitaka watoto waliobahatika kupata kujifunza wenyewe kupokewa na kuendelezwa zaidi.

Kauli hiyo pia imetolewa na mzazi mwingine Janeth Massawe ambaye alisema mradi huo ni wa mfano kwani umewasaidia kuwaondolea tatizo la elimu katika eneo lao. Alisema mradi huo umepokewa vyema na kwamba umewachagiza kutambua umuhimu wa elimu.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (kushoto), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (katikati) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (katikati) funguo za gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo (kulia), Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (katikati) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto), Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu (wa pili kulia), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kulia).
 Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (aliyeshika usukani) na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi  wakiwa ndani ya gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP mara baada ya kupokea gari hilo kutoka UNESCO wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mgeni rasmi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Zena Said akitoa hotuba wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za UNESCO wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo akifafanua jambo wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli , Bi Odilia Mushi akizungumza wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mtoto Habiba Athumani (13) mkazi wa kijiji cha Tabora wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Mtoto Ismail Adamu (13) mkazi wa kijiji cha Majengo wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Stella Ernest ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Hassan Shomari ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na wazazi ambao watoto wao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Baadhi ya watoto ambao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wadau wa sekta ya elimu walioshiriki katika hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos wakitiliana saini na Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) ya hati ya makabidhiano ya mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa kufunga mradi huo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto  wa halmashauri ya Korogwe walionufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad