VICTOR MASANGU, MKURANGA
KILIO cha muda mrefu ambao kilkuwa kinawakabili wakulima wa zao la
muhogo katika Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani hatimaye hivi karibuni
wanatarajia kuondokana na changamoto sugu ya upatikanaji wa soko la
uhakika kufuatia kuanza kwa ujenzi wa mradi wa kiwanda kikubwa
cha kuchakata zao hilo ambacho kitagharimu kiasi cha shilingi bilioni
9.5
Hayo yamebainishwa na baadhi ya wakulima hao wakati wa Ziara ya kikazi
ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wakati wa halfa ya
uwekeaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho ambacho kimejengwa na
mwekezaji kutoka nchini China katika kijiji cha Mkenge kata ya Beta
Wilayani Mkuranga ambapo wamedai hapo awali walikuwa na tatizo la
kuuza mihogo yao kwa bei ya hasara.
“Sisi kama wakulima wa zao hili la muhogo katika Wilayah ii ya
mkuranga tumefarijika sana kwa ujio wa mradi w akiwanda hiki ambacho
kimejengwa na marafiki zetu wa kutoka nchini chini, na tunashukuru kwa
jitihada ambazo zinafanywa na Mkuu wetu wa Mkoa wa Pwani pamoja na
Rais wetu Dk. John Pombe Magfuli kwa kuwaleta wawekezaji hawa ambao
watatusaidia kuondokana na tatizo la kupata soko la uhakika,”walisema
wakulima hao.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo
amewataka maafisa kilimo wote kuhakikisha wanatimiza wajibu wao
ipasavyo kwa kuwasimamia vema wakulima wa zao hilo la muhogo
kutonyonywa na walanguzi na kupata haki zao stahiki na kuahidi
kuwaondoa kazini wale wote ambao watabainika kukwamisha juhudi za
serikali katika uwekezaji sekta ya viwanda.
Aidha Ndikilo alisema kuwa lengo kubwa la serikali ya awamu ya tano ni
kuhakikisha inawasaidia kwa hali na mali wananchi wake katika
kuondokana na changamoto mbali mbali ambazo zinawakabili ikiwemo
ukosefu wa masoko ya ukakiha, ajaira hivyo aatahakikisha zao hilo la
muhogo linapata soko kupitia viwanda ambavyo vinajengwa na waekezaji
katika maeneo mbali mbali na kuwahimiza wasikate tama na badala yake
waendelee zaidi kulima mazao ya biashar ikiwemo ufuta,muhogo na
korosho.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga amesema
kuwa kipindi cha nyuma wakulima wengine walikuwa tayari wameshakata
tamaa katika kilimo cha zao la muhogo,hivyo kumamilika kwa kiwanda
hicho kitaweza kuleta mabadili chanya kwa kuwapa fursa wananchi kuwa
na soko la uhakika .
“Kwa kweli wananchi wangu hasa kwa wakulima wa zao hili la muhogo
katika Wilaya ya Mkuranga baadhi yao walikuwa tayari wameanza kukata
tama kabisa na kujikitza zaidi na kilimo cha zo la muhogo nah ii hali
ni kutokana na mfumo ambao ulikuwepo wanauza mazao yao kwa bei ya
hasara kweli lakini kwa sasa kiwanda hiki kinakamilika mwaka huu hivyo
wataondokana kabisa na changamoto ya soko,”alismema Sanga.
Awali akisoma Risala ya ujenzi wa mradi huo mmoja wa vongozi wa
kiwanda Leonard Jambeli kwa niaba ya Mkurugenzi amebainisha kwamba
waanategemea kutoa fursa za ajira za moja kwa moja kwa wazawa zaidi
ya mia moja pindi uzalishaji utakapoanza kufanyika rasmi.
KUKAMILIKA kwa mradi huo wa ujenzi wa kiwanda mwishoni mwa mwaka huu
kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa wakulima wa zao hilo katika
halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ambao kwa miaka mingi
walikuwa wanapata hasara kutokana na kunyonywa na walanguzi kununua
zao hilo kwa bei ndogo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo kushoto akipeana mkono wa pongezi na Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha kuchakata zao la muhogo mara baada ya halfa ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho amabcho kimejengwa katika kijiji cha Mgenge kata ya Beta Wilayani Mkuranga,(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mkuu wa Mkoa wa Pwani kushoto Mhandisi Evarist Ndikilo akipata maelekezo kutoka kwa mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha kuchakata muhogo wakati alipofanya ziaara yake ya kikazi kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akiwa kaatika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi mbali mbali wa kiwanda hicho cha kuchakata muhogo mara baada ya kumalizika kwa zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi.
Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kushoto Ramadhani Maneno akimshika mkono Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ikiwa ni moja ya ishara ya kumpongeza katika juhudi zake za kuunga mkono juhudi za serikali katika ujenzi wa viwanda
Mmoja wa viongozi wa kiwanda hicho cha kuchakata zao la muhogo kulia Leonard Jambeli akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani kabla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho pembeni yake kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza
na baaadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho pamoja na watumishi mbali
mbali wa serikalini, pamoja na wananchi wa wa kijiji cha Mkenge hawapo
pichani katika halfa fupi iliyoandaliwa kwa lengo la uwekezaji wa
jiwe la msingi kataika kiwanda hicho.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
No comments:
Post a Comment