HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 13, 2019

SONGAMBELE NA NAISINYAI ZAFAIDIKA NA ZIARA YA DKT BASHIRU

MATAWI ya Chama Cha Mapinduzi ya Naisinyai na Songambele Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara yamepatiwa mabati 200 na Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally kwa ajili kujenga ofisi mpya za matawi hayo. 

Dk Bashiru akizungumza na wanachama wa matawi hayo alisema mabati hayo yanatolewa kupitia mfuko wa kuendeleza chama wa Mwenyekiti wao Rais John Magufuli. 

Alisema uhai wa chama hicho unategemea wanachama waliopo kwenye matawi na mashina hivyo wanayaunga mkono ili kuendelea kuifanya CCM iwe karibu zaidi na wananchi. 

Pia, aliwapongeza baadhi ya wadau wa maendeleo wa mji mdogo wa Mirerani, Paul Mollel na Siria Mepukori kwa kila mmoja kuchangia sh500,000 ya ujenzi wa tawi la CCM Songambele na diwani wa kata ya Loiborsiret Ezekiel Lesenga (Mardad) alijitolea mifuko 20 ya saruji kwa tawi la Songambele. 

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alijitolea mifuko 100 ya saruji ya tawi la Songambele, mbunge wa jimbo la Simanjiro, James Ole Millya alijitolea mifuko 40 kwenye tawi la Naisinyai na mifuko 20 ya saruji katika tawi la Songambele. 

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Yefred Myenzi alisema yeye binafsi anachangia mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa tawi la CCM Songambele. 

Mbunge wa jimbo la Simanjiro James Ole Millya alisema amewatafutia wadau na amewachangia kwani matawi yote ni ya kwake, Naisinyai ni CCM yote japo hapo Songambele diwani ni Chadema.

Kada wa chama hicho Siria Mepukori alisema yeye ni mdau wa maendeleo na aliamua kumuunga mkono Dk Bashiru kwa sh500,000 ili  kufanikisha ujenzi wa tawi hilo la Songambele.

Kada mwingine Paul Mollel alisema amechangia sh500,000 kwenye ofisi hiyo ya Songambele ili kumuunga mkono Katibu Mkuu wa CCM ambaye ana lengo zuri la kuhakikisha matawi yanajengwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akizungumza na wanachama wa CCM wakati wa kuzindua Tawi la Oloshonyokiye Kijiji cha Naisinyai Wilayani Simanjiro na kuipatia mabati 100.
 Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akishiriki ujenzi wa Tawi la Songambele Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara na kuipatia mabati 100.
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akipokewa na viongozi mbalimbali alipowasili Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad