HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 13, 2019

Prof. Kabudi akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Prof. Palamagamba J. Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mikhail Bogdanov, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Shirikisho la Urusi katika Ofisi Ndogo ya Wizara Jijini Dar es Salaam. Wamezungumzia masuala mbalimbali yaliyolenga kuboresha na kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya mataifa haya mawili, hususan, katika Nyanja ya kidiplomasia, nishati, biashara na uwekezaji. Naibu Waziri huyo yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Mawaziri wanaendelea na mazungumzo hayo, huku ujumbe aliofuatana nao Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi ukifuatilia mazungumzo hayo 
utoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mej. Jenerali mstaafu Simon Mumwi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga, Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Mhe. Yuri Popov na Afisa wa Ubalozi wa Urusi nchini Tanzania wakifuatilia mazungumzo ya Mawaziri. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad