Na Ahmed Mahmoud Arusha
Serikali za Canada na Tanzania zinaendesha mradi wa miaka mitano wenye lengo la kusaidia vijana kuweza kuwa na umahiri wa kujiajiri na kujifunza kwa kutenda.
Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa vyuo vya ufundi nchini Dkt.Noel Mbonde wakati akifungua semina ya mradi huo inayoendelea jiji Arusha na kubainisha kuwa mradi huo utafikia malengo ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa Kati wa viwanda.
Amesema kuwa mradi huo ulionza mwaka 2014 unatarajiwa kufika tamati Machi mwakani utasaidia Sana vijana kwani unalenga kumuwezesha kijana na mwalimu kuwa karibu na umeleta mabadiliko chanya nchini.
"Serikali imejipanga kuhakikisha mradi huu unakuwa endelevu baada ya kumalizika kwani tuna miradi mingi inaendeshwa nchini yenye lengo la kuongeza weledi kwa vijana wetu kuweza kufikia adhma ya serikali ya uchumi wa Kati wa viwanda"alisema Dkt.Mbonde.
Kwa upande wake mwakilishi wa Balozi wa Kanada nchini Tanzania bi Nathalie Garon amesema kuwa serikali ya nchi yake itaendeleza ushirikiano wa dhati kuhakikisha vijana wa kitanzania wanafikia malengo endelevu na nchi inapiga hatua.
Amesema MAFUNZO hayo ni moja ya ushirikiano Kati ya nchi yake na serikali ya Tanzania kuonyesha jinsi wanavyothamini vijana katika suala zima la KUKUZA maendeleo ya bara la Afrika.
Mwakilishi
wa balozi wa Canada nchini bi Nathalie Garon ambaye pia ni karibu wa
Kwanza wa maendeleo na kiongozi wa ukiaji endelevu wa uchumi wa ubalozi
huo akifungua semina ya mradi wa kusaidia vyuo vya ufundi nchini
unaondelea. Kwenye chuo cha Veta njiro jijini Arusha picha na Ahmed
Mahmoud Arusha.
Mkurugenzi
wa elimu ya ufundi wizara ya elimu na ufundi Dkt.Noel Mbonde
akizungumza kwenye semina ya mradi wa kusaidia vyuo vya ufundi nchini
iliyofanyika kwenye chuo cha Veta Njiro jijini Arusha picha na Ahmed
Mahmoud Arusha
Tom
Tunney meneja mradi wa ushirikiano na serikali za Canada na Tanzania
kuhusu mafunzo ya kukuza maarifa kwenye sekta ya ajira rasmi na isiyo
rasmi akitoa mada kwenye semina ya mafunzo yaliowakutanisha wakuu wa
vyuo vya ufundi (veta) inayofanyika jijini Arusha picha na Ahmed Mahmoud
Arusha.
No comments:
Post a Comment