HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 30, 2019

WADAU WA AFYA KUTAFUTA UFUMBUZI WA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU KWA WATOA HUDUMA WA SEKTA YA HIYO

 Mkurugenzi wa chuo cha madaktari wasaidizi  Ifakara mkoani Morogoro Prof. Frola Kessy akielezea changamoto ya  wahudumu wa afya katika kutoa takwimu sahihi na namna ya kuepuka na changamoto hiyo katika mkutano wa wadau wa afya mkoani Morogoro.
 Wadau wa afya na wakufunzi kutoka vyuo  mbalimbali hapa nchini ikiwemo chuo kikuu cha Mzumbe, chuo kikuu cha Dodoma, kituo cha kimataifa cha mafunzo ya afya Ifakara na chuo kikuu cha Mhimbili  wakifatilia kwa umakini mjadala wa namna takwimu zinazokusanywa jinsi ambavyo zinavyoshindwa kutumiwa ipasavyo na wahudumu wa afya.
 Mtakwimu mkuu ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa(TAMISEM) Yasinta Kijuu akiwasilisha kwa wadau wa afya namna ambavyo serikali iliona mifumo ya takwimu usivyotumiwa ipasavyo  na kuangalia jinsi   ya kutatua changamoto hiyo  katika mkutano wa wadau wa afya uliofanyika mkoani Morogoro ambapo alisema  mwaka 2016 ndipo mchakato wa kutatua changamoto hiyo ya matumizi ya takwimu  ulianza.
 Wadau wa afya wakimfatilia kwa umakini katika mkutano wa wadau wa afya mkoani Morogoro mkufunzi wa chuo kikuu Mzumbe Dr,Mackfallen Anasel akizungumzuia jinsi ambavyo mitaala ya kufundishia inahitaji marekebisho katika swala la ukusanyaji na matumizi ya takwimu  ili wahitimu  wa vyuo waelewe  matumizi sahihi ya takwimu hizo .
Makamu  mkuu wa chuo taaluma,utafiti na ushauri kutoka chuo cha serikali za mitaa  Hombolo Dodoma  Dr, Michael Msendekwa akitoa ushauri wa jinsi gani ya kufikia utoaji wa huduma sahihi za afya kwa wananchi na jinsi ya kuodoa vikwazo vinavyo kwamisha  matumizi sahihi ya takwimu katika kutoa maamuzi  katika kikao cha wadau wa afya mkoani Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad