HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 19, 2018

NHIF YATUMIA MAAFALI YA SHULE YA MSINGI KANA CENTRAL ENGLISH MEDIUM KUTOA ELIMU YA TOTO AFYA KADI

 MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza wakati wa mahafali ya 8 ya Darasa la Saba katika Shule ya Kana Eglish Medium Central  School ya Jijini Tanga ambapo alitumia nafasi hiyo kuhamasisha mpango wa Toto Afya Kadi kwa watoto na wazazi.
 Afisa Uanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Nico Kasebwa kushoto akisisitiza jambo kwa mmoja wa wananchi wa Jiji la Tanga aliyefika kwenye banda lao kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko huo uli kuweza kunufaika na huduma za matibabu wakati wanapougua kushoto ni Afisa Uanachama NHIF Jesca Nyau
 Afisa Uanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Nico Kasebwa akimuonyesha kitu kwenye kipeperushi chenye maelezo ya Mpango wa Toto Afya Kadi mkazi wa Jiji la Tanga Daudi Mbisco mara baada ya kutembelea banda lao
 Sehemu ya wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo
 Sehemu ya Wazazi na Walezi wakiwa kwenye Mahafali hayo

MFUKO wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) umewapa mbinu bora za wazazi na walezi kuwapa zawadi muhimu watoto wao katika maisha yao ni kuwaingiza kwenye mpango wa Toto Afya kadi ili waweze kunufaika na huduma za matibabu.

Hayo yalisemwa na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga Ally Mwakababu wakati akizungumza na wanafunzi na walezi kwenye mahafali ya nane ya darasa la Saba katika shule ya Kana Central English Medium Primary School.

Alisema wakati wa ukuaji wa watoto wamekuwa wakikumbana na magonjwa mbalimbali ambayo yanaweza kupelekea kukwamisha ndoto zao lakini wanapokuwa wameandikishwa kwenye mpango wa Toto Afya Kadi wanaweza kupata matibabu kwenye vituo mbalimbali vya Afya.

“Nimekuja hapa kwa lengo kuu moja kuhamaisha umuhimu wa wazazi na walezi kuwapa zawadi ya Bima watoto wao kupitia mpango wa Toto Afya Kadi kwani hakuna anayweza kuelezea gharama za matibabu wakati mtoto wake anayweza kuungua”Alisema.

Hata hivyo alisema kwamba wazazi wanapowaingiza watoto wao kwenye mpango huo unawapa uhakika wa matibabu na wanaweza kuwa na kumbukumbu nzuri ya maisha yao .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad