HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 26, 2018

TADB KUONGEZA NGUVU TANTRADE KULIVAA SOKO LA CHINA

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ipo katika mpango mkakati wa kuungana na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) katika kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo kuchangamkia fursa za uwepo wa soko la uhakika la mazao ya kilimo nchini China ili kuongeza tija katika kilimo biashara nchini.

Hatua hii ya TADB ni kuitikia wito wa fursa za uwepo wa soko la uhakika wa mazao ya kimkakati yaliyomwayo nchini kama ilivyobainika wakati wa maonyesho ya 15 ya ASEAN (CAEXPO) 2018 yaliofanyika wiki iliyopita huko Nanning, Guangxi nchini China ambako Tanzania ilipewa heshimiwa kuwa mshirika maalum wa maonyesho kutoka barani Afrika.

Akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya TADB na TANTRADE kilicholenga kujadilia namna Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania itakavyoweza kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo kuchangamkia fursa za uwepo wa soko la uhakika la mazao ya kilimo nchini China, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine amesema TADB ipo tayari kuwawezesha kwa kuwapa mikopo ya gharama nafuu ili kupata mtaji wa uhakika katika kuongeza tija shughuli za kilimo.

“Tumejipanga kuitikia wito huu kwa vitendo kwa kuzingatia kuwa moja kati ya majukumu ya benki ni kusaidia kuwaunganisha wakulima na masoko ili kuinua uzalishaji wenye tija katika Sekta ya Kilimo nchini,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade,, Bw. Edwin Rutageruka amesema TanTrade ilipeleka sampuli mbalimbali za mazao na bidhaa za Tanzania katika Maonesho ya Kimataifa ya CAEXPO 2018 ambapo Tanzania imepata fursa ya soko kwa mazao zaidi ya 10 ikiwemo korosho, kahawa, mbaazi, choroko, degu, chai, tangawizi, asali na mhogo.

“Wakati wa CAEXPO 2018  bidhaa zilizosindikwa kutoka Tanzania zilipata soko kubwa hivyo tunadhani ujio wa TADB utsaidia kuongeza nguvu za kimtaji ili kuweza kukidhi mahitaji ya kimtaji kwa wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya kilmo,” alisema.

Bw. Rutageruka aliongeza kuwa maonyesho hayo yaliwashirikisha zaidi ya wafanyabiashara wakubwa 50 kutoka China ambao wameonesha nia ya kufanya biashara na Tanzania hasa katika mazao ya kilimo.

kwa mujibu wa taarifa ya mwaka 2017 ya Benki Kuu ya Tanzania, China ni nchi ya nne katika nchi zinazonunua bidhaa kutoka Tanzania ambapo ilinunua takribani asilimia 8 ya bidhaa zote zilizouzwa nje ya Tanzania kwa mwaka 2016/2017.
 Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka (kushoto) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) wakati walipokutana katika kikao cha pamoja kati ya TADB na TANTRADE kilicholenga kujadilia namna Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania itakavyoweza kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo kuchangamkia fursa za uwepo wa soko la uhakika la mazao ya kilimo nchini China.
 Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka (kulia) akizungumza juu ya fursa za masoko nchini China wakati wa kikao cha pamoja kati ya TADB na TANTRADE. Anayemsikiliza ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kushoto).
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine akifafanua jambo wakati wa kikao.
 Washiriki wa majadiliano hayo wakiwa katika picha ya pamoja.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka (kulia) mara baada ya kikao cha pamoja kati ya TADB na TANTRADE kilicholenga kujadilia namna Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania itakavyoweza kuwawezesha wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo kuchangamkia fursa za uwepo wa soko la uhakika la mazao ya kilimo nchini China.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad