HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 29, 2018

BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAKUTANA KUJADILI USALAMA WA CHAKULA NA MASOKO KWA WAKULIMA

Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utetezi kutoka ACT Bw Timothy Mmbaga akichangia mada kwenye Mkutano wa wadau wa Kilimo uliokuwa ukijadili usalama wa Chakula na Masoko kwa wakulima ulioandaliwa na Baraza la Kilimo chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania (TAP) uliofanyika jana mjini dodoma. 
Katibu Tawala Msaidizi Sekta za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Dodoma Bi Aziza Mumba akichangia Mada kuhusu Nafasi ya NFRA na CPB katika kuimarisha Usalama wa Chakula, Bei za vyakula na Masoko kwa wakulima ulioandaliwa na Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania (TAP) uliofanyika jana Mjini Dodoma
Mratibu wa taifa wa ubia wa kilimo Tanzania TAP, Bw. Mark Magila akichangia mada wakati wa mkutano wa wadau wa kilimo uliokuwa ukizungumzia usalama wa chakula na masoko kwa wakulima ulioandaliwa na baraza la kilimo Tanzania chini ya mradi wake wa TAP na kuhudhuliwa na wadau mbalimbali wa kilimo uliofanyika mjini Dodoma jana. 
Sehemu ya washiriki wa warsha ya wadau wa kilimo nchini wakifuatilia kwa ukaribu mjadala wa nafasi ya NFRA na CPB katika kuimarisha usalama wa chakula bei za vyakula na masoko ya wakulima, ulioandaliwa na Baraza la Kilimo Tanzania ACT, Chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania TAP, uliofanyika jana mjini Dodoma.
Afisa Sera kutoka Baraza la Kilimo Tanzania (ACT), Bi Laetitia Wiliam akisikiliza kwa makini uwasilishwaji wa Mada ya iliyokuwa ikihusu Nafasi ya NFRA na CPB katika kuimarisha Usalama wa Chakula, Bei za vyakula na Masoko kwa wakulima, katika walisha iliyoandaliwa na ACT chini ya Mmradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania (TAP) uliofanyika jana Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utetezi kutoka ACT Bw Timothy Mmbaga akiwa katika Picha ya pamoja na baada ya kumalizika kwa Mkutano wa wadau wa Kilimo uliokuwa ukijadili usalama wa Chakula na Masoko kwa wakulima ulioandaliwa na Baraza la Kilimo chini ya Mradi wake wa Ubia wa Kilimo Tanzania (TAP) uliofanyika jana mjini dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad