HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 20, 2018

VIONGOZI WA NGAZI MBALIMBALI,WANANCHI WASHIRIKI KATIKA MAZISHI YA BABA YAKE MZAZI SALMA KIKWETE MAKABURI YA KISUTU

Na Hadija Seif,Globu ya Jamii
VIONGOZI wa ngazi mbalimbali Serikalini , viongozi wastaafu pamoja na mamia ya wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wameshiriki katika mazishi ya mzee Rashid Mkwachu ambaye ni baba yake mzazi Mke wa Rais mstafu Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete.

Mwili wa mzee Mkwachu umezikwa leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mzee Mkwachu alifikwa na umauti Julai 19 mwaka huu  na chanzo cha kifo chake kimeelezwa na Msemaji wa familia ya Kikwete,Ridhawani Kikwete kuwa mzee huyo amefariki kutokana na magonjwa ya utu uzima kwani umri wake ulikuwa zaidi ya miaka 100.

Kabla ya mwili kufikishwa makaburi ya Kisuti ibada na dua kumuombea marehemu mzee Mkwachu zilifanyika nyumbani kwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete Msasani jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya viongozi walioshiriki kwenye maziko hayo ni Rais Mstaafu Al haji Ali Hassan Mwinyi,  Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa.

Akizungumza kwenye msiba huo Sheikh Mkuu wa Tanzania Muft Abuubakary Zubeiry amesema maisha ya binadamu ya kuishi kwenye ulimwengu ni mafupi sana na kwa kawaida ni kati ya miaka 63 na ikitoa zaidi ya hapo ni zawadi tu.

Amesema kuwa viumbe vyote ni vinamuda wake wa kuondoa kwenye huu ulimwengu na hakuna ambaye ataishi milele na kufafanua na kufa si kutoweka moja kwa moja bali ni utaratibu wa maisha ya kutoka kwenye ulimwengu na kwenda akhera.

Kwa upande wake Mjuukuu wa Marehemu Mzee Mkwachu ambaye pia ni Msemaji wa Familia Ridhwan Kikwete alieleza kilichokuwa kikimsumbua babu yake ni magonjwa ya utu uzima.

Ametumia nafasi hiyo kuwashukuru woye ambao wamepata nafasi kwa namna moja a nyingine kuungana nao katiki kipindi hiki ambacho cha majonzi wako.

Waombolezaji walioungana katika maziko ya Baba mzazi wa mke wa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Mtoto wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Ridhiwan Kikwete akitoa salamu za shukrani kwa waombolezaji waliounga nao katika maziko ya  Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete akiaga mara baada ya kumaliza maziko ya  Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiaga mara baada ya kumaliza maziko ya Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Rais Mstaafu awamu ya pili Mhe. Alhaji Al-Hassan Mwinyi akiaga mara baada ya kumaliza maziko ya Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwaaga marais wastaafu wa pili Mhe. Alhaji Al-Hassan Mwinyi (katikati) na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete mara baada ya mara baada ya kumaliza maziko ya  Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.
Rais Mstaafu awamu ya pili Mhe. Alhaji Al-Hassan Mwinyi akiaga na aliyekuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova mara baada ya kumaliza maziko ya Baba mzazi wa Mama Salma Kikwete, Mzee Rashid Mkwachu, aliyefariki dunia jana Alhamisi, Julai 19, 2018, ambapo maziko ya marehemu yamefanyika katika Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo Julai 20, 2018.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad