Monday, August 10, 2015

USHINDI WA VETA KATIKA MAONESHO YA KILIMO (NANENANE) KITAIFA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kusini Mashariki, Bw. Joseph Kibehele kikombe cha ushindi baada ya VETA kuibuka Mshindi wa Kwanza katika eneo la Taasisi za Mafunzo na Utafiti kwenye Kilele cha Maonesho ya Kilimo (Nanenane) kitaifa,  iliyofanyika viwanja vya Ngongo, mkoani Lindi, tarehe 8 Agosti, 2015.
 Wafanyakazi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) wakiwa katika picha ya pamoja kufurahia ushindi baada ya VETA kuwa Mshindi wa Kwanza kwenye eneo la Taasisi za Mafunzo na Utafiti katika kilele cha Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kitaifa, kwenye viwanja vya Ngongo, mkoani Lindi. Aliyeshika kikombe ni Mwenyekiti wa Bodi ya VETA Kanda ya Kusini Mashariki, Br. Sixtus Luoga.
 Wafanyakazi wa VETA wakishangilia kikombe cha ushindi baada ya VETA kutunukiwa Ushindi wa Kwanza kwenye eneo la Taasisi za Mafunzo na Utafiti katika kilele cha Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kitaifa, kwenye viwanja vya Ngongo, mkoani Lindi.

No comments:

Post a Comment