HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 25, 2014

UNAKUMBUKA SHERIA HIZI ZA SOKA LA MCHANGANI ENZI ZILE ZA UTOTO......??

 Wakati wa Makuzi yetu enzi zile,ilikuwa ni lazima ukutane na mambo hayo hapo chini hasa katika mchezo wa mpira wa miguu.nayo ni kama ifuatavyo:-

1.Mwenye mpira lazima acheze hata kama hajui kucheza mpira

2.Dogo mnene lazima awe golikipa

3.Mwenye mpira ataamua nani acheze na nani asicheze kwenye mtanange huo.

4.Kama haujashiriki kutafua mifuko ya kutengenezea mpira unaweza usipate namba siku zotee

5.Ukichaguliwa mwishoni ujue uwezo wako ni mdogo kuliko wote kwenye kabumbu.
6.Mwenye mpira akikasirika basi ujue na mpira umeisha

7.Mwenye mpira anaruhusiwa kubadili golikipa,kama kuna penati imetokea baada ya hapo ataendelea kudaka yule yule.....

8.Mechi itaisha pale giza linapoingia

9.Wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufata mpira ukitoka wakati wa mchezo

10.Yule mtaalam wa soka huwa hakosi namba hata siku moja..!
 
Haya jikumbushe ndugu Mdau na kana unakumbukumbu zozote za aina hii usisite kututumia kupitia Email yetu : 
othmanmichuzi@gmail.com

Ukiikumbuka lazima utabasamu tu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad