

“mkutano huo utatoa nafasi kwa Tanzania kuonyesha fursa za uwekezaji zilizopo katika Tasnia ya kuku na ndege wafugwao kuongeza wigo wa masoko ya bidhaa hizo katika nchi za SADC na kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi za SADC katika Tasnia hiyo” amesema Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe ameshukuru uongozi wa awamu ya sita uliochini ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele na kufungua fursa za wawekezaji katika sekta za uzalishaji ikiwemo Tasnia ya Kuku.
Vilevile, Prof. Shemdoe amesema tukio hilo litaambatana na maonesho ya kitaifa ya Tasnia ya kuku na ndege wafugwao yatakayofanyika 18-19 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar Es Salaam.
Prof. Shemdoe amesema, mgeni Rasmi katika mkutano huo ni Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko.
No comments:
Post a Comment