HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 26, 2015

MKUTANO MKUBWA WA AMANI NA UPENDO KUFANYIKA LEO JIJINI ARUSHA

SAM_3390
SAM_3402Askofu Solomon Mwagisa ambaye ni katibu wa mkutano wa Amani na Upendo utakaofanyika leo jijini Arusha katika viwanja vya reli kwanzia saa 8 mchana hadi saa 12 jioni akielezea namna walivyojiandaa na mkutano huo,kushoto ni Askofu Mkuu wa makanisa ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini kati Solomon Massangwa(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_3404Askofu Mkuu wa makanisa ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini kati Solomon Massangwa akizungumza na wanahabari jana jijini hapa kuhusu mkutano huo mkubwa wa Amani na Upendo ambapo alisema kuwa ni muhimu kwa kila mtu kuhakikisha Amani inakuwepo huku akisisitiza kuwa bila Amani hakuna kitu chochote kinachoweza kufanyika pasipo Amani
SAM_3407Paul Malisa mwakilishi wa Askofu mkuu Josephat Lebulu wa kanisa Katoliki Arusha ,Paroko wa Parokia ya mtakatifu Theresia Arusha mjini akizungumza na wanahabari juu ya mkutano huo ambapo alisema kazi walionayo ni kuhakikisha wanapigia debe Amani hasa katika kipindi hichi kuelekea uchaguzi mkuu
SAM_3401Eng.Tunzo Muzava ambaye ni mratibu wa mkutano huo akizungumza na vyombo vya habari jana alisema kuwa Muhubiri mkubwa wa kimataifa kutoka Marekani Will Graham anatarajiwa kuhubiri katika mkutano huo huku kwaya zaidi ya 200 kutumbuiza,Mkutano huo unashirikisha makanisa yote ya Arusha

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad