Monday, September 24, 2012

PPF kwa Kushirikiana na Bw. Pieter Naut watoa msaada kwa kituo cha watoto yatima Kigogo


 
Mkurugenzi wa Maswala ya TEHAMA wa PPF Pensions Fund, Bw. Robert Mtendamema (Katikati), meneja mafunzo wa Kampuni ya Laserfiche kutoka Marekani,Pieter Naut (Watatu kulia) ni afisa uhusiano wa Mfuko huo,Ms. Janet Ezekiel, wakigawa vifaa kwa watoto yatima wakituo cha New Life Orphanage Centre kilichoko Kigogo Randa Bar jijini Dar es Salaam jana. Msaada huo ulitolewa na Nauta ambaye alikuwa nchini kutoa mafunzo ya IT kwa wafanyakazi wa PPF ambapo wanatumia system hiyo. System hiyo hutumika kutuma document kutoka Idara mmoja kwenda nyingine bila kuzunguka na mafile. System hii imepunguza matumizi ya karatasi. 
Mkurugenzi wa Maswala ya TEHAMA wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,Bw. Robert Mtendamema, akizungumza kwenye hafla ya kutoa msaada kwa watoto yatima wa kituo cha New Life, Kigogo jijiji Dar Es Salaam jana.Katikati ni meneja mafunzo wa Kampuni ya Laserfiche kutoka Marekani , Pieter Naut akifuatiwa na Meneja Uhusiano wa Mfuko wa pensheni wa PPF, Bi.Lulu Mengele. 
 
Bw. Robert Mtendamema (Kushoto), akizungumza jambo na meneja mafunzo wa Kampuni ya Laserfiche kutoka Marekani, Pieter Nauta, wakati wakitoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa kituo cha kulea watoto hatima cha New Life , Kigogo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment