Haya
ni magogo yaliyokuwa yamevunwa isivyo halali katika msitu wa Ngumburuni, Msitu
huu upo wilaya ya Rufiji, Mkoa wa Pwani.
Miti hii ilikatwa kwa ajili ya uchomaji wa mkaa.
Msitu huu wa asili na misitu
mingine mbalimbali nchini imekuwa ikivamiwa na kuvunwa isivyo halali kwa
kiwango cha kutisha kwa faida ya watu wachache. Magogo haya yalikamatwa na
wanavijiji wa kijiji cha MUYUYU moja ya vijiji vinavyozunguka msitu huu baada ya juhudi zao za kuomba msaada
wa kukomeshwa kwa uvunaji haramu kutoka ofisi ya wilaya kushindikana.
Baada ya
juhudi hizo kushindikana waliamua kutumia vyombo vya habari mbalimbali ili
kufikisha malalamiko yao ngazi za juu zaidi..
Baada ya taarifa kutoka kwenye
vyombo vya habari, wavunaji haramu ambao wanatumia vyombo vya kisasa kuchakata
magogo walikimbia na kuacha magogo msituni. Wanakijiji walichangishana fedha na
kuzomba magogo kutoka msituni na kuleta kijijini. LAKINI UHARIBIFU MKUBWA AMBAO
UNGEWEZA KUDHIBITIWA TOKA AWALI ULIKWISHA TOKEA.
Tutambue kuwa misitu hii inaharibika huku tukiwa
na taasisi mbalimbali ambazo zimepewa jukumu la kusimamia misitu yetu vizuri,
taasisi hizi zinawafanyakazi ambao ndio wamepewa jukumu hilo. Changamoto kubwa
ni kwamba kumekuwa na wafanyakazi wachache wasiokuwa waaminifu na hivyo kushirikiana na wahalifu
kuharibu misitu yetu huku nchi ikikosa pia mapato..
Hii haikubaliki,
haikubaliki wananchi wanaojitolea bure bila malipo kuisaidia serekali kusimamia
misitu yake wanatoa taarifa kwa mamlaka iliyopewa dhamana ya kusimamia mistu
kisheria na mamlaka hizo kupuuza huku misitu yetu ikiendelea kuharibiwa kila kukicha.
Imefika wakati sasa
kila afisa wa msitu/misitu kuwajibika kutokana na hali ya misitu wanayopewa
kuisimamia. Kama hawatawajibishwa maana yake hawataweka juhudi zozote
kuhakikisha wanailinda misitu yetu vizuri..
Afisa misitu anapopewa taarifa za
uvunaji wa kutisha ndani ya msitu aliopewa jukumu la kuusimamia na kutochukua
hatua stahiki kwa visingiziao visivyokuwa na mashiko tumuelwe vipi?
Tukisema
anashirikiana na wavunaji haramu kuhujumu misitu yetu tutakuwa tunakosea? Wakala
wa misitu, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wasaidie kuhakikisha watumishi wao
wanatenda kazi yao inavyostahili.
Mkuu wa mkoa wa Tanga ametuonyesha mfano wa
namna ya kuwawajibisha watendaji wake kwa kumshtaki mwenyekiti wa kijiji kwa
kosa la kutochukua hatua zozote huku msitu uliopo kijijini kwake ukiteketea kwa
uchomaji wa mkaa. Mamlaka nyingine zinaweza, Hii ndio tafsiri ya uwajibikaji
kwa vitendo.


No comments:
Post a Comment