Friday, August 24, 2012

SEKESEKE LA SENSA YA WATU NA MAKAZI.

 Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiisilamu nchini Sheikh Ponda Issa Ponda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu zoezi la Sensa linalotarajiwa kufanyika Augost 26 mwaka huu, ambapo alisema waisilamu kamwe hawatashiriki zoezi hilo na watakaa itikafu misikitini usiku wa Augost 25 na kusoma dua mpaka asubuhi.
 Masheikh zaidi ya 40 ktoka kwenye taasisi na jumuiya na mabaraza ya kiisilamu nchini ambao pia ni maimamu wa misikiti mbalimbali jijini Dar es Salaam wakiwa wakimuunga mkono Katibu wa taasisi na Jumuiya za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda wakati akitangaza maelekezo kwa waisilamu juu ya namna ya kuwajibu makalani wa sensa.

No comments:

Post a Comment