"Wachimbaji wadogo wamekuwa wakileta marudio yao hapa na kuondoka na dhahabu safi kwa haraka. Hii inathibitisha umuhimu wa kuwawekea miundombinu mizuri na teknolojia rafiki," alisema Dkt. Kiruswa.
Akizungumza wakati huo huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Subira Mgalu, aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa kipaumbele wachimbaji wadogo. Alitoa wito kwa STAMICO na Wizara ya Madini kuongeza na kupanua vituo vya mfano ili kuwafikia wachimbaji wengi zaidi kwa haraka.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO, Deusdedith Magala, aliwashukuru wajumbe wa Kamati kwa kuridhika na uwekezaji wa Shirika hilo unaolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa jamii.






No comments:
Post a Comment