IGP Wambura amesema hayo Jijini Tanga wakati akifunga Kikao cha Watendaji wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka mikoa ya Tanzania bara na Zanzibar kilichokuwa kikifanyika jijini humo kwa siku tatu kwa lengo la kufanya tathmini kwa mwaka 2022 na kuweka mikakati kwa mwaka 2023.
Aidha, aliwataka watendaji hao kuhakikisha kuwa kunaendelea kuwepo na usiri katika kushughulikia wahanga wa vitendo vya ukatili nchini na kwa wanaofanya vitendo hivyo waweze kufichuliwa ili lengo la kukomesha vitendo hivyo liweze kutimia sambamba na watendaji hao kujenga taswira chanya ya Jeshi la Polisi kwa jamii jambo ambalo litasaidia kutoa haki kwa Wahanga wote wa matukio hayo.
No comments:
Post a Comment