VITUO ATAMIZI KUWA KICHOCHEO CHA MABADILIKO SEKTA YA MIFUGO NCHINI - MTAA KWA MTAA BLOG

HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 15, 2022

VITUO ATAMIZI KUWA KICHOCHEO CHA MABADILIKO SEKTA YA MIFUGO NCHINI

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki, akizungumza na washiriki wa MafunzoRejea ya Maafisa Ugani wa Kanda ya Mashariki wakati akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Pwani jana Desemba 13, 2022. 

Na Mbaraka Kambona, Pwani 

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema kuwa Wizara yake imeanzisha vituo atamizi kuwawezesha vijana kufuga kwa tija ili kujikwamua kimaisha na pia kuwa ni kichocheo kwa wafugaji wengine kujifunza kwa vitendo na kubadilika kutoka katika ufugaji wa kienyeji na kufanya ufugaji wa kisasa utakaowaletea tija zaidi na kupunguza migogoro isiyo ya lazima kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.

Ndaki aliyasema hayo wakati akifunga Mafunzo Rejea kwa Maafisa Ugani wa Kanda ya Mashariki yaliyofanyika mkoani Pwani jana Desemba 13, 2022.

Alisema kuwa Wizara yake imewekeza na inahamasisha Vijana kushiriki katika uzalishaji wa mifugo kupitia Vituo Atamizi ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 vijana 240 waliohitimu vyuo vya Mafunzo ya Mifugo wamedahiliwa na kuanza mafunzo ya unenepeshaji wa ng’ombe katika vituo nane (8).

“Kwa mantiki hiyo nawahimiza wadau mbalimbali kuwekeza na kuhamasisha vijana kujiunga na Vituo atamizi ambavyo vimeanzishwa na Wizara kwa sababu vijana hao wakimaliza mafunzo hayo watasaidia wafugaji wengine kubadilika na kuanza kufuga kwa tija,” alisema Ndaki.

“Mwakani tunatarajia kuwa na vijana wengi zaidi kwa sababu tutaongeza bajeti kuhusu vituo hivi ili tuweze kuwachukua vijana wengi zaidi hata kufikia 1000, kwa sababu vijana hawa wakitawanyika kote nchini wataleta mageuzi kwenye ufugaji wetu,”alifafanua 

Aidha, alisema kuwa huduma za ugani ni kiungo muhimu kati ya watafiti na wafugaji ili kupata ufugaji wenye tija hivyo ni vyema maafisa ugani wakaimarisha mahusiano mazuri ili waweze kufikia malengo tarajiwa.

“Nitoe rai kwenu kujenga ushirikiano madhubuti baina yenu na wafugaji utakaowezesha kutoa taarifa sahihi, kusambaza teknolojia, kuelimisha, kutoa ushauri wa kitaalamu na kupata mrejesho,”alisema.

Waziri Ndaki alisema kuwa wanatambua  changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya mifugo hususan katika utoaji wa huduma za Ugani hapa nchini lakini tayari Wizara kupitia Mpango wa Mabadiliko wa Sekta ya Mifugo imebainisha mikakati na afua mbalimbali za kuzipatia suluhisho changamoto hizo.

“Miongoni mwa juhudi za serikali ni pamoja na kuanza kutoa Mafunzo Rejea kwa Maafisa Ugani Watakaowafundisha Wengine (Trainer of Trainee) ambapo jumla ya Maafisa Ugani 800 watafikiwa kwa mwaka wa fedha, 2022/2023. Aidha, Wizara inatarajia kutoa mafunzo elekezi kwa wafugaji 182,200 nchini ambapo ninyi mtatusaidia sana katika kutekeleza jukumu hilo,”alifafanua.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad