Ubaguzi wa kijinsia ni mwiko
kwa Benki ya NMB na juhudi zake za kutokomeza kabisa unyanyapaaji huo
nchini zimeiheshimisha duniani na kupelekea harakati zake za kupambania
usawa wa kijinsia kazini kuthibitishwa rasmi kimataifa.
Benki
hiyo imetunukiwa na taasisi ya The Edge Certified Foundation hati
maalumu ya kutambulika rasmi duniani kama kinara katika mgawanyo wa
kiuchumi kwenye suala la kijinsia (EDGE Certification) miongoni mwa
taasisi za kifedha barani Afrika.
NMB ni ya kwanza kupata
mafanikio hayo kitaasisi kwenye nchi zote zilizoko kusini mwa Jangwa la
Sahara. Bw Akonaay alisema zipo taasisi nyingine mbili ambazo si za
kifedha zenye hati hiyo za Kaskazini mwa Afrika (Moroco na Misri).
Aidha,
tafiti zimedhibitisha kuwa uwiano wa kijinsia ni kichocheo kizuri cha
ubunifu na ukuaji wa kiuchumi, kuimarika kwa shughuli za uzalishaji mali
na kuwepo utulivu wa kifedha na uwiano wa kipato.
Pia NMB
inatambua kuwa swala hili ni miongoni ya vipaumbele vya Malengo ya
Maendeleo Endelevu (SDGs) ya Umoja wa Mataifa. Bw Akonaay alisema
umuhimu wake kimaendeleo ni pamoja na kuzingatia ukuaji wa biashara za
kibenki.
Alibainisha faida nyingine za cheti cha EDGE Access
ambayo ni hatua ya kwanza ya taasisi kuelekea kufanikiwa kuutokomeza
kabisa ubaguzi wa kijinsia ni pamoja na NMB kutambulika kama muajiri
anayezingatia masuala ya usawa wa kijinsia kazini.
Naye,
Mwakilishi wake mkazi, Bw Frank Ajilore, alisema usawa wa kijinsia
kazini kuna faida nyingi kibiashara na kiuchumi kwani akina mama
wakiwezeshwa wanachangia vizuri kasi ya maendeleo.
Benki ya NMB
yenye wafanyakazi zaidi ya 3,500 imepiga hatua kubwa kwenye eneo hili na
uwiano wake wa kijinsia umepanda kutoka asilimia 45 wanawake na
asilimia 55 wanaume mwaka 2015 hadi asilimia 48 kwa 52 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment