HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 2, 2019

SERIKALI IMESHAURIWA KUCHUKUA HATUA ZA HARAKA ILI KUDHIBITI TATIZO LA VIFO VYA WAJAWAZITO NCHINI

 MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati akizinduzi wa kimkoa wa kampeni ya uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi mkoa wa Tanga ijulikanayo “jiongeze tuwavushe salama”
 KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi akizungumza katika uzinduzi hu
 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita akizungumza wakati wa uzinduzi huo
 MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akichangia jambo kwenye uzinduzi huo
 MKUU wa wilaya ya Korogwe Kissa Gwakisa akizungumza wakati wa uzinduzi huo
 MKUU wa wilaya ya Handeni Godwin Gondwe akizungumza jambo
  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita kushoto akiwa na Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah mara baada ya uzinduzi huo ambao uliwenda sambamba na uwekaji saini ahadi
  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita kushoto akiwa na Mkuu wa wilaya ya Korogwe Kisa Gwakisa mara baada ya uzinduzi huo ambao uliwenda sambamba na uwekaji saini ahadi
 MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akifuatilia utiaji wa saini na kuweka ahadi Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah
  MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Gissa Gwakisa akisaini

 Wakuu wa wilaya wakifuatilia kwa umakini uwasilishwaji wa taarifa mbalimbali kwenye uzinduzi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah,Mkuu wa wilaya ya Korogwe Kissa Gwakisa,Mkuu wa wilaya ya Lushoto January Lugangika na Mkuu wa wilaya ya Kilindi Sauda Mtondoo
 KATIBU Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim kulia akiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza Desderi Haule wakifuatilia kwa umakini uzinduzi huo
 Katibu wa Afya Mkoani Tanga Abdiely Makange kulia akisisitiza jambo na mmoja wa washiriki wakati wa uzinduzi huo
 Sehemu ya washirki wa uzinduzi huo wakimsikiliza kwa umakini mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella


SERIKALI imeshauri kuchukuwa hatua za haraka ilikuweza kudhibiti tatizo la vifo vya wajawazito nchini kuepuka kupoteza nguvu kazi kubwa ambayo ingeweza kuwa msaada mkubwa kwa uchumi wa nchi.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela wakati Uzinduzi wakampeni ya uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi mkoa wa Tanga ijulikanayo “jiongeze tuwavushe salama”

Alisema kuwa takwimu za vifo vya wajawazito inaonyesha vinazidi kukuwa kila siku hivyo wakati umefika sasa wa kuhakikisha serikali inashughuli kwa haraka changamoto hizo ili kuweza kupunguza vifo hivyo.

“Kwa mkoa wa Tanga pekee kwa kipindi cha mwezi mmoja tayari wajawazito nane wamepoteza maisha hivyo kwa takwimu hizo inamaana mpaka mwisho wa mwaka kutakuwa na vifo vingi “alisema RC Shigela.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Zena Said alisema kuwa miongoni mwa changamoto kubwa ni ukosefu wa miundombinu bora ya afya kama vile gari la wagonjwa pamoja na uhaba wa wataalamu .

Vile vile alisema kuwa changamoto nyingine mama mjamzito kutokwa na damu nyingi,pamoja na kutopatiwa usaidizi wa haraka pindi pale anapokuwa amefikishwa katika kituo cha afya kwa ajili ya huduma.

Hata hivyo Mganga Mkuu wa mkoa Dkt Asha Mahita aliweza kutaja takwimu za vifo kwa kipindi cha miaka minne ambapo kwa mwaka 2015 jumla ya vifo vilikuwa 67.

“Kwa mwaka 2016 kuliuwa na vifo 46 ,huku mwaka 2017 kukiripotiwa vifo 45,ambapo mwaka 2018 kukiwa na vifo 54”alibainisha Mganga Mkuu huyo.

Aidha alisema kuwa mikakati iliyokuwepo ni kupeleka elimu kwa jamii kuona umuhimu wa kuhudhuria cliniki kwa wakati,kushughulia kwa haraka changamoto za vifo vitokanavyo na uzazi.

“Tumejipanga katika kuhakikisha kila wilaya, huduma ya mama na mtoto inakuwa ni kipaumbele chetu lakini pia kutenga bajeti kubwa ili kuweza kutatua kwa haraka changamoto za wajawazito na watoto wachanga”alisema Dkt Mahita.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad