HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, January 22, 2019

VIFO NA MATUKIO YA AJALI ZA BARABARANI YAPUNGUA MKOANI PWANI -KAMANDA WANKYO

NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 
MATUKIO ya ajali za barabarani yamepungua mkoani Pwani, kutoka ajali 91 zilizotokea mwaka 2017 hadi kufikia ajali 62 zilizotokea kipindi cha mwaka 2018. Aidha mwaka 2017 watu waliokufa kutokana na ajali hizo ni 88 ,na mwaka 2018 ni watu 58 .

Akitoa taarifa ya makosa ya usalama barabarani kimkoa, katika kipindi cha mwaka uliopita, kamanda wa polisi mkoani Pwani, (ACP) Wankyo Nyigesa alisema waliojeruhiwa ni watu 136 katika kipindi cha mwaka 2017 na mwaka 2018 waliojeruhiwa ni 97 .

"Kupungua kwa vifo na ajali zitokanazo na matukio ya ajali za barabarani haimaanishi madereva waendelee kukiuka sheria za usalama barabarani"..La hasha,"nawataka watii sheria hizo na watumiaji wengine warekebishe na kuvifanyia matengenezo vyombo vyao vya moto kabla ya kuviweka barabarani "alisema Wankyo. 

Wakati huo huo, alieleza hali ya uhalifu katika kipindi cha 2018 yamepungua ukilinganisha na mwaka 2017 ambapo matukio 2,327 yaliripitiwa katika vituo mbalimbali vya polisi wakati 2017 matukio 2,478 yaliripotiwa.  "Kwa takwimu hizi tumepunguza matukio  151 makubwa kwa mwaka 2018 ikilinganishwa na mwaka 2017 "alieleza Wankyo. 

Wankyo alibainisha, wanaendelea kupambama na mabasi yanayosafiri kupitia barabara za mkoa wa Pwani kwa kuyakagua na kuona kama yana ubora wa kufanya usafirishaji wa abiria. "Kudhibiti ujazaji ndani ya mabasi, uzidishaji wa nauli kwa abiria kwa kushirikiana na SUMATRA, malori na kuyafanyia ukaguzi wa kina katika maeneo yao ya maegesho na yanapopita kwenye barabara zetu "alisisitiza. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad