Shirikisho la Soka Barani Afrika, CAF limetoa taarifa ya kusogeza mbele tarehe ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2019 yatakayofanyika nchini Misri;..
Hatua hii inakuja baada ya Shirikisho hilo kutaarifiwa na waandaaji wa michuano ya AFCON , Misri, kwamba tarehe iliyopangwa awali inaingiliana na mwezi wa mtukufu wa Ramadhan hivyo inaweza kuathiri viwango vya wachezaji wa kiislam, Mwezi mtukufu wa Ramadhani unatarajiwa kuanza Jumapili ya Mei 5 na kukamilika Jumanne ya Juni 4,
Awali, AFCON 2019, ilipangwa kuanza Juni 14 na kumalizika Julai 13 lakini sasa imesogezwa mbele kwa takribani wiki moja, ambapo itaanza Juni 21 na kumalizika Julai 19.
CAF imeripoti kwamba droo ya michuano hiyo ya kwanza kabisa kushirikisha timu 24, itafanyika xcsdAprili 12 mwaka huu, majuma machache baada ya mechi za mwisho za kufuzu zitakazofanyika mwezi Machi.
Misri ilipata haki ya kuandaa michuano hiyo baada ya waandaaji wa awali, Cameroon kushindwa kuiridhisha CAF kwa maandalizi yake.
No comments:
Post a Comment