HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, January 27, 2019

MAKAMU WA RAIS ASHEHEREKEA SIKU YA KUZALIWA NA WATOTO WALIOZALIWA LEO HOSPITALI YA RUFAA MOROGORO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Januari 27 kwa kushirikiana na Benki ya NMB, wametoa Vifaa Tiba vya kujifungulia katika wodi ya Mama na Mtoto, pamoja na vifaa tiba hivyo aliwazawadia  watoto 36 waliozaliwa siku ya  katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro .

Makamu wa Rais aliwakilishwa na Katibu wake Bw. Juma S. Mkomi ambaye amesema kuwa Makamu wa Rais amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha huduma ya afya ya mama na mtoto inaboreshwa.

“Suala la kuboresha huduma ya mama na mtoto limeelezewa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 lakini Makamu wa Rais kwa upekee amelipa kipaumbele kwa sabau ni moja kati ya ahadi zake kuu wakati kampeni” alisema Katibu huyo wa Makamu wa Rais.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Rita Lyamuya amemshukuru Makamu wa Rais kwa kuwakumbuka watoto waliozaliwa hospitalini hapo ambapo alisema kuwa watoto 36 wamezaliwa katika siku ya leo na kwa kipindi cha robo mwaka watoto  1779 walizaliwa  kati ya hao waliozaliwa kwa upasuaji ni 586.

Aidha, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki Aikansia Muro amesema Benki ya NMB inaunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika kuboresha huduma zote za kijamii hususani sula zima la  afya na elimu na wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za kijamii ambapo leo wamemuunga mkono Mhe. Makamu wa Rais kwa kutoa Vitanda vinne vya kujifungulia, Vifaa vya kumsaidia mama kujifungulia (delivery kit) 8, pamoja na vifaa vingine ambavyo kwa ujumla vinagharimu shilingi milioni 5.

Kwa Upande mwingine Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro Bw. Clifford Tandari ameishukuru Serikali kwa kutenga shilingi bilioni 8.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali 3 na vituo vya afya 11 katika mkoa wa Morogoro.
  Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akimkabidhi Bi. Apendae Mohamed (kushoto) beseni yenye mahitaji muhimu kwa mtoto wake  ikiwa zawadi kutoka kwa  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa katika hospitali ya Rufaa ya Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akimkabidhi Bi. Apendae Mohamed (kushoto) akipokea kadi kwa niaba ya   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kukabidhi zawadi  kwa watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa kwa Makamu wa Rais katika hospitali ya Rufaa ya Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akipokea Vifaa Tiba vya kujifungulia wakina mama kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki Bi. Aikansia Muro ikiwa sehemu ya Benki hiyo kuunga mkono juhudi za Makamu wa Rais katika kuboresha huduma ya afya ya Mama na Mtoto leo katika hospitali ya rufaa ya Morogoro ambapo Makamu wa Rais alitoa zawadi kwa watoto 36 waliozaliwa tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
  Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Lucy Nkya moja ya mabeseni yenye mahitaji muhimu kwa watoto waliozaliwa leo ikiwa zawadi kutoka kwa  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Lucy Nkya akionyesha juu moja ya mabeseni yenye mahitaji muhimu kwa watoto waliozaliwa leo kama ishara ya kumshukuru Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka  watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari ikiwa ni kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad