HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 12, 2018

Mastercard na M-Pesa wazindua kadi inayowezesha kufanya manunuzi mtandaoni


Kaimu Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi (Kati), Raisi wa Kusini mwa Sahara wa Mastercard, Raghay Prasad (kushoto) na Mkuu wa hazina na kitengo cha soko la kimataifa wa Banki ABC, Barton Mwasamengo (kulia) wakionesha ushirikiano kati ya M-Pesa na Mastercard uliozinduliwa jana jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi (Kati), Raisi wa Kusini mwa Sahara wa Mastercard, Raghay Prasad (kushoto) na Mkuu wa hazina na kitengo cha soko la kimataifa wa Banki ABC, Barton Mwasamengo (kulia) wakionesha ushirikiano kati ya M-Pesa na Mastercard uliozinduliwa jana jijini Dar es Salaam.

 Kwa mtu yeyote aliyewahi kufanya manunuzi ya kitu chochote bila kuinuka kitini ama kutoka nyumbani kwake anaweza kuelezea urahisi na wepesi wa kufanya manunuzi mtandaoni, lakini hii imekuwa ni ndoto kwa Watanzania walio wengi, mpaka sasa ambapo Mastercard wameungana na Vodacom na BancABC kutengeneza kadi ya kwanza itakayowezesha manunuzi mtandaoni – M-Pesa Virtual Card.

“Huduma ya M-Pesa kutoka Vodacom ina wateja Zaidi ya milioni 8.2 huku ikiwa na Zaidi ya wakala laki moja waliotapakaa nchi nzima, hii inawezsha upatikanaji wa uhakika wa huduma za kifedha, lakini imekuwa ni ngumu pale linapokuja suala la kulipia manunuzi mtandaoni haswa kupitia tovuti za kimataifa. Uzinduzi na ufanyaji kazi wa Virtual Card kupitia M-Pesa utaleta mapinduzi katika kuwezesha Watanzania kufanya manunuzi mtandaoni na kuondosha vikwazo ikiwamo kuwa na akaunti ya benki na pia hatari ya mteja kuweka taarifa zake za kibenki mtandaoni,” alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc Hisham Hendi.

Inategemewa kwamba uunganisho wa intaneti kwa bara la Afrika itaongezeka sana ikiwa ni matokeo ya upatikanaji wa simu janja (Smartphone) na pia ukuaji wa utoaji huduma yenye kasi zaidi ya intaneti kutoka kwa watoa huduma kama Vodacom. Ongezeko hili la upatikanaji wa huduma ya intaneti litaongeza uhitaji wa maudhui ya kidijitali, mitandao ya kijamii, M-Commerce, elimu ya mtandaoni na pia malipo mtandaoni kurahisishwa na kuongezewa usalama zaidi.

Kadi hii itawawezesha wateja wa M-Pesa kufanya malipo ya aina yeyote kwa tovuti za kimataifa au za hapa nyumbani, ama kwa kutumia zana (App) yeyote ambayo inatumia na Mastercard kwa malipo, bila kuhitajika kuwa na akaunti ya benki au kadi ya mkopo (Credit Card). Wateja wanaweza kutengeneza virtual card kupitia menyu ya M-Pesa ama kupitia App yetu ya M-Pesa (huduma hii tutaiongeza hivi karibuni) na kuijaza pesa kupitia mfumo wetu wa M-Pesa. Kadi hii inakuwa tayari kwa matumizi mara tu baada ya kujazwa pesa.

“Muendelezo wa kusambaza teknolojia iliyovumbuliwa katika biashara za kimtandao inawakilisha fursa kubwa zilizomo katika huduma jumuishi za kifedha, hii inamaanisha kwamba watu wengi zaidi wataweza kufanya malipo bila kuwa na pesa mkononi. Malipo ya ina hii yanategemewa kuwa zaidi ya asilimia 60, hii inathibitisha kwamba kwa baadaye huduma jumuishi za kifedha bila shaka zitakuwa kwenye simu zetu za mikononi ambazo tunakuwa nazo kila mahali,” alisema Raghav Prasad, Rais wa Mastercard kwa divisheni ya ukanda wa Sahara.

Malipo rahisi na salama mtandaoni imethibitishwa kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha, Tanzania imepiga hatua kubwa katika huduma za kifedha katika miaka kumi iliyopita: asilimia ya Watanzania wanaoshikilia sehemu ya uchumi wa nchi ilikuwa ni asilimia 15.8 mwaka 2009 lakini idadi hiyo ilipanda hadi asilimia 65.3 mwaka 2017, ongezeko hili linatokana na kuanzishwa kwa huduma rahisi za kifedha kupitia simu za mkononi kama M-Pesa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad