HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 13, 2018

Taasisi ya RSA yafanya Kongamano mkoani Dodoma

 Baadhi ya Mabalozi wa Usalama barabarani pamoja na wadau wa Usalama barabarani wakiwa katika kongamano la siku moja Bungeni Dodoma katika Ukumbi wa Pius Msekwa. Picha na Vero Ignatus.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi ambae pia alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahengeakizungumza katika kongamano la Usalama. Barrabarani lililoandaliwa na Mabalozi wa usalama barabarani( RSA) na kufanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Dodoma jana. Picha na Vero Ignatus
 Mwalimu wa Elimu ya Usalama barabrani ambae pia ni mmoja wa Baraza la Usalama. Barabarani Nchini. Picha na Vero Ignatus
 Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe akizungumza katika kongamano hilo Jijini Dodoma. Picha na Vero Ignatus
Henry Bantu kutoka Baraza la Usalama barabarani Nchini akizungumza na mabalozi katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Dodoma. Picha na Vero Ignatus.
Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria Nchini Marlin Komba Akiwa na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Nchini Fortunatus Musilim. Picha na Vero Ignatus. 
 Wa kwanza kushoto ni mwenyekiti wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Nchini (RSA) John Seka akifuatiwa na Kamanda wa Polisi Kikosi chq Usalama Barabarani SACP Fortunatus Musilim, Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe, Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini Patrobas Katambi, Mkuu wa Polisi kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Iringa Kamotta, na Mkurugenzi wa Huduma ya sheria Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Marlin Komba. Picha na Vero Ignatus. 
Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe akiwa na mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi 
Wakiwa wameshikilia bango lenye maandishi yasemayao Tunataka mabadiliko ya sheria ya Usalama barabarani Nje ya Ukumbi wa Bunge Pius Msekwa jana. Picha na Vero Ignatus. 
Mkurugugenzi wa Huduma ya sheria Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Marlin Komba akisalimiana na mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe, Bungeni Dodoma jana. Picha na Vero Ignatus
Wakwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Mabalozi wa Usalama barabarani Nchini John Seka, katikati ni Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Huduma ya Sheria Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Marlin Komba. Picha na Vero Ignatus. 


Na. Vero Ignatus Dodoma. 

Taasisi ya mabalozi wa usalama barabarani nchini wamefanya kongamano la siku Mkoani Dodoma dhima kuu ikiwa '' Mabadiliko ya sheria ni muhimu katika kuimarisha usalama nchini''

Kongamano hilo limefanyika kwasababu ya mkono mabadiliko ya sheria za usalama barabarani kushirikiana /kuwahusisha viongozi wanaohusika na mambo ya kisera na waunge mkono mabadiliko ya sheria hiyo. 

Mkurugenzi wa habari na mawasiliano RSA, ambae pia ni mjumbe wa Baraza la Taifa usalama barabarani Augustus Fungo amesema kuwa wanahitaji mabadiliko ya sheria ya usalama barabarani kwani iliyopo haikidhi na imepitwa na wakati kwani ilitungwa mwaka 1983. 

'' Wakati sheria hii ikitungwa sayansi na teknolojia ilikuwa haijashika kasi kama ilivyo sasa, barabara zetu, vyombo vya moto vilikuwa vichache tofauti na miaka ya leo'' alisemaFungo

Kwa upande wake Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Tanzania Fortunatus Musilim amewapongeza RSA kwa ushirikiano wao na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa mbalimbali pale ajali inapotokea na hata pale sheria zinapovunjwa hata uhalifu unapotokea. 

Amesema kuwa ajali nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva, vyombo vya usafiri kuwa vibovu (haswa malori) miundo mbinu ya barabara. 

'' Tayari tumeanzisha operasheni inayoendelea nchi nzima ya kukagua leseni kwa madereva katika stendi za mabasi na uhakiki wa vyeti ili kutambua kama dereva hiyo amepata mafunzo''Alisema Kamanda. 

Mkuu wa wilaya ya Gairo Siriel Mchembe amewataka mabalozi hao wa usalama barabarani kutoa elimu chanya kwa wananchi na kuzima elimu hasi inayowashuka askari wa usalama. Barabarani wakati wanatimiza majukumu yao. 

"ukimuona askari anawavusha watoto au wapitanjia kwa ujumla usiwadharau kwani kazi yake kubwa ni kuhakikisha jamii inakuwa salama

Amesema kuwa nchi haitoweza kuwa ya viwanda kama watu watakuwa wanapata ulemavu unaotokana na ajali za barabarani. 

Mkuu wa wilaya ya dodoma. Mjini Patrobas Katambi ambae pia alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa dodoma  Dkt Binilith Mahenge  amesema changamoto Kubwa ya usalama barabarani ufahamu mdogo walionao. Maderwva na haswa wakati wa utoaji wa leseni kwani wanapeqa. Watu wasiokuwa sahihi. 
Ajali inaepukika.









Matukuo mbalimbali kama inavyoonekanq pichani katika Kongamano la siku moja lililofanyika Jijini Dodoma katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni. Picha na Vero Ignatus. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad