HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 13, 2018

MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI 2018

Wakulima wakipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa kilimo wa halmashauri ya Wilaya ya Momba katika banda la maonyesho ya nanenane, juu ya njia rahisi ya kupanda mboga za majani kwa kutumia magunia na mifuko hususan mahali pasipo na maeneo ya kupanda bustani.
Mhifadhi wa Mazingira na kilimo hai kutoka Wilaya ya Songwe Noah Ambokile Mbilinyi akitoa maelezo kwa Eddie Mhelela kuhusu aina mpya ya maboga ambayo yana uzito wa Kilogramu 15 mpaka 25 katika banda la wilaya ya Songwe kwenye maonyesho ya nanenane.
Mwanzilishi wa kikundi cha kutunza Mazingira cha Estate Vision Amani Zakaria Elias akitoa maelezo kwa baadhi ya wananchi waliojitokeza katika banda la maonyesho ya Nanenane katika halmashauri ya Wilaya ya Ileje, kikundi hicho kimeonyesha upekee kwa kuweka miche ya miti ya mtini na mizeituni ambayo ni adimu kupatikana.
Afisa Kilimo kutoka shirika la Norwegian Christian Aid Daniel Isaack akitoa maelezo katika maonyesho ya nanenane kuhusu teknolojia rahisi ya umwagiliaji wa matone ambayo inaweza kutumia maji lita 20 kumwagilia miche 52 ya mbogamboga, wakulima takriban 50 wa wilaya ya Mbozi wameanza kutumia teknolojia hii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad