HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 16, 2018

MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA AKABIDHI ZAWADI MASHINDANO YA MASAUNI-JAZEERA VISIWANI ZANZIBAR

 Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James (wapili kulia), Mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni, Nassoro Salim Jazeera (wakwanza kulia) na Mbunge wa jimbo hilo wakiwakabidhi kombe wachezaji wa timu ya Miembeni baada ya kuibuka washindi katika mchezo wa fainali ya Mashindano ya Masauni-Jazeera kwa kuifunga timu ya Kilimani bao 1-0.Mchezo huo umefanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Kikwajuni visiwani Zanzibar.
 Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM), Kheri James  (kulia),akimkabidhi nahodha wa timu ya Kilimani, zawadi ya mipira baada ya kuibuka washindi wa pili  katika mchezo wa fainali ya Mashindano ya Masauni-Jazeera .Katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni. Mchezo huo umefanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,Kikwajuni visiwani Zanzibar.
 Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM), Kheri James, akionyesha fedha  kabla ya kuwakabidhi washindi wa Fainali ya Mashindano ya Masauni-Jazeera ambapo timu ya Miembeni iliibuka na ushindi wa bao 1-0.Wakwanza kulia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni Nassoro Salim Jazeera na watatu ni Mbunge wa Jimbo hilo, Mhandisi Hamad Masauni. Mchezo huo umefanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,Kikwajuni visiwani Zanzibar.
 Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wachezaji na mashabiki waliofika kushuhudia mchezo wa fainali ya Mashindano ya Masauni- Jazeera uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Kikwajuni Visiwani Zanzibar, ambapo timu ya Miembeni walibuka mabingwa baada ya kuifunga timu ya Kilimani bao 1-0.
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar, Dk. Abdulla Juma Saadalla, akizungumza na wachezaji na mashabiki waliofika kushuhudia mchezo wa fainali ya Mashindano ya Masauni- Jazeera uliofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Kikwajuni Visiwani Zanzibar, ambapo timu ya Miembeni walibuka mabingwa baada ya kuifunga timu ya Kilimani bao 1-0.Wengine meza kuu ni Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM), Kheri James na Mbunge wa Jimbo la Kiwajuni,Mhandisi Hamad Masauni.  
Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James(kulia) na Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni,Mhandisi Hamad Masauni, wakiteta jambo wakati wa fainali ya Mashindano ya Masauni- Jazeera iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad