HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 12, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje Kushiriki Maadhimisho ya siku ya Afrika

Mazungumzo yakiendelea.






Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Grace Mujuma amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wa nchi za Afrika wanao wakilisha nchi zao hapa nchini,Mabalozi hao ni kutoka nchi za Namibia na Malawi, pamoja na mambo mengine katika mazungumzo hayo walijadiliana kuhusu maadhimisho ya kumbukumbu ya siku ya Umoja wa Afrika.

Umoja huo ulioanzishwa Mwaka 1963 kwa lengo la kutetea maslahi mbalimbali ya Bara la Afrika, kuongeza umoja zaidi katika kutetea uhuru na kulinda mipaka yake. Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Namibia Mhe. Theresia Samaria, akimwelezea Balozi Mujuma (hayupo pichani), namna wanavyotarajia kuadhimisha hafla hiyo kwa hapa nchini, kulia ni Balozi wa Malawi Mhe. Hawa Olga Ndilowe akimsikiliza kwa makini.

Sehemu ya watumishi waliohudhuria mazungumzo hayo, wa kwanza kulia ni Bw. Salvatory Mbilinyi, Bw. Makamba Dahari na mwisho kushoto ni Bi. Zulekha Tambwe .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad