HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 17, 2018

SPIKA WA BUNGE AFANYA MAZUNGUMZO NA WABUNGE WA IRELAND LEO JIJINI DODOMA

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (katikati) na Mbunge wa Bunge la Ireland, Mhe. Catherine Conolly (kulia) walipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Wabunge wa Bunge la Ireland walioambatana na Maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Ireland walioongozwa na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kushoto kwake) walipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Ireland ambao pia ni Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland, walioongozwa na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kulia) baada ya mazungumzo nao yaliyofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland wakutana na kuzungumza na Mtandao wa Wabunge wanawake wa Bunge la Tanzania (TWPG) leo katika Ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland katika tukio lililofanyika leo nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa Jijini Dodoma. Lengo likiwa ni kujenga urafiki na kubadilishana uzoefu katika utendaji wao wa kazi.

(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad