JAMII
imeaswa kujenga misingi imara ya malezi ya watoto ili wasiweze kuishi
maisha ya mitaani na ambayo yanasababisha kokosa haki za kupata elimu
pamoja na malezi mengine.
Hayo
ameyasema leo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga wakati akizindua ripoti ya Taifa ya
Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania, amesema kuwa
sehemu salama ya kuishi watoto ni katika familia au jamii.
Amesema
kuwa katika ripoti hiyo watoto wa kike wamekuwa wakionekana katika
majira ya usiku wakijiuza huku watoto wakiume wanaonekana majira ya
mchana na usiku.
Nkinga
amesema kuwa serikali itafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo ili
katika kuweza kuhakikisha watoto hao wanakwenda katika familia zao.
Amesema
sababu zinazowafanya watoto kuishi na kufanya kazi mitaani ni
umasikini pamoja na ukatili wa kupindukia na kuamua baadhi ya watoto
kutoroka katika familia zao na kuingia mitaani.
“Jamii
iendelee kuishi kwa amani na misingi bora katika malezi ya watoto
katika kuhakikisha hawakimbilii mitaani kwa kuishi kwa kukosa chakula,
elimu pamoja wengine kupoteza maisha kutokana na kupigwa “amesema
Nkinga.
Ripoti
hiyo inatoa matokeo ya utafiti wa watoto wenye umri kati ya miaka 0-18
ambao wanaishi mitaani na kufanya kazi katika miji sita nchini kwa
hesabu wanaoishi usiku na mchana kwa watoto wanaoishi mitaani na
kufanya kazi wakati wa mchana 6,393 na usiku 1,385 kwa wavulana
waliohesabiwa mchana ni asilimi 76 ya watoto wote wasichana walifikia
asilimia 24 wakati mchana na usiku kwa wasichana iliongezeka na kufikia
asilimia 30 wakijihusisha na ngono huku asilimia hiyo ikipungua kwa
asilimia 70 wakati wa usiku .
Mapendekezo
ya ripoti hiyo ni kwa serikali na wadau wengine kuhakikisha kwamba
watoto wanaoishi nakufanya kazi mitaani kuwaungnisha katika mifumo ya
ulinzi wa watoto katika ngazi zote za kitaifa na kiwilaya.
Mkurugenzi
wa Railway Afrika, Peter Kent amesema kuwa kazi yao ni kutaka watoto
kurudi katika familia zao na kuendelea kuishi huku wakiwa wanafatilia
kuhakikisha haki za msingi wanazipata.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Sihaba Nkinga akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya
Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo
jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Sihaba Nkinga akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya
Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo
jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Railway Afrika, Peter Kent akizungumza na waandishi wa habari juu ya
mikakati ya shirika hilo katika masuala ya watoto wanaoishi na kufanya
kazi mitaani wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi
na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es
Salaam.
Naibu
Mwakilishi Mkazi USAID Kizazi Kipya Project wa PACT Tanzania, Levina
Kikoyo akizungumza jinsi ya utafiti waliofanya katika ripoti hiyo.
Sehemu
ya wadau mbalimbali wa masuala ya watoto waliohudguria katika uzinduzi
wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini
Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Sihaba Nkinga akiwa na wawakilishi wa mashirika wakati wa uzinduzi ya
Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania
uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment