UJENZI wa mradi wa maji Shizuvi kijiji cha NyalaIlembo Halmashauri ya wilaya Mbeya mkoani Mbeya uliotekelezwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa),umekamilika kwa asilimia 100 na hivyo kumaliza kabisa kero ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama iliyokuwepo kwa wakazi wa kijiji hicho kabla na baada ya Uhuru.
Mradi huo umetekelezwa kwa gharama ya Sh.milioni 482 kupitia fedha za mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ugonjwa wa Uvico-19, utahudumia takribani wakazi 2,474.
No comments:
Post a Comment