Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi amewaalika wafanyabiashara kutoka China washirikiane naye kuwekeza nchini kwa ubia katika miradi mbalimbali, wakati huu ambapo Tanzania inapojizatiti kuwa ya viwanda.
Dr Mengi ametoa rai hiyo jijini Dar es salaam wakati wa chakula cha mchana alichowaandalia wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji, walioambatana kwenye hafla hiyo na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke.
Amesema Tanzania ni nchi iliyojaaliwa fursa nyingi za uwekezaji kutokana na utajiri wake wa raslimali na kusisitiza kuwa waliotayari kushirikiana naye katika miradi mbalimbali kama ya ujenzi wa bomba la gesi kutoka Tanzania hadi Uganda wajitokeze.
Akizungumza katika hafla hiyo Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke amesema ofisi yake itakuwa kiunganishi baina ya Wafanyabiashara wa China na Dr Mengi katika kufanikisha pendekezo la kuanzisha kwa ubia hapa nchini viwanda mbalimbali.
Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara hao Bw. Lyu Xinhua amesema amekuja na ujumbe kutoka makampuni 17 ya China yanahusika na shughuli mbalimbali kuanzia ujenzi wa miundombinu, uhandisi, teknolojia ya mawasiliano nk, na kuahidi kuwasilisha mapendekezo yaliyotolewa kwa makampuni husika kwa ajili ya hatua zaidi za utekelezaji.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akiwa ameambatana na
Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke mara baada ya kuwasili wakati wa
hafla ya chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa wawakilishi wa
makampuni 17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji
iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akiongozana na Kiongozi
wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua kuelekea
kwenye eneo maalum kushiriki hafla ya chakula cha mchana kilichoandaliwa
Dr. Mengi kwa wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo nchini
kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel
jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akizungumza wakati wa
chakula cha mchana alichowaandalia wawakilishi wa makampuni 17 kutoka
China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi
iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha
kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Tanzania Private
Sector Foundation (TPSF), Bw. Louis Accaro, Kiongozi wa Ujumbe wa
wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua, Balozi wa China nchini
Mhe. Wang Ke, Mkurugenzi Mtendaji wa IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha
pamoja Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe.
Balozi
wa China nchini Mhe. Wang Ke akizungumza machache kabla ya kumkaribisha
Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua
kutoa salamu wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa
wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa
za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es
Salaam. Wengine katika picha ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP
Dr. Reginald Mengi (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa IPP Touchmate,
Bw. Victor Tesha (wa pili kulia) pamoja Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw.
Godfrey Bitesigirwe (kulia).
Kiongozi
wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua akitoa salamu
kwa niaba ya ujumbe huo wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa
Dr. Mengi kwa wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo nchini
kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel
jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP
Dr. Reginald Mengi
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akimshukuru Balozi wa
China nchini Mhe. Wang Ke kwa kumtambulisha vyema wakati wa chakula cha
mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa wawakilishi wa makampuni 17 kutoka
China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi
iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akipokea
zawadi kutoka kwa Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China,
Bw. Lyu Xinhua wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi
kwa wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo nchini kutafuta
fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel jijini
Dar es Salaam.
Sehemu
ya wafanyabiashara wawakilishi wa makampuni 17 kutoka China waliopo
nchini kutafuta fursa za uwekezaji waliposhiriki hafla fupi ya chakula
cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi iliyofanyika Serena Hotel jijini
Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi (katikati) akiwa kwenye
picha ya pamoja na Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China,
Bw. Lyu Xinhua pamoja na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke wakati wa
hafla ya chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa wawakilishi wa
makampuni 17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji
iliyofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akiwa katika picha za
kumbukumbu na baadhi ya wafanyabiashara kutoka China waliopo nchini
kutafuta fursa za uwekezaji wakati wa hafla ya chakula cha mchana
kilichoandaliwa Dr. Mengi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es
Salaam.
No comments:
Post a Comment