HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 7, 2018

WAHITIMU MAJENGO SEC. 2000 WASAIDIA YATIMA, DAR, MWANZA NA KILIMANJARO

Mmoja wa wakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro, Eng. Willbard Gandu (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada wa wanafunzi hao katika kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro, Injinia Eng. Maeda (kulia) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam sehemu ya msaada uliotolewa na wanafunzi hao.
Mmoja wa viongozi wa kundi hilo la wanafunzi waliohitimu Sekondari ya Majengo, Joachim Mushi (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha watoto yatima ‘Green Pastures’, Mchungaji Douglas Kiseu sehemu ya msaada uliotolewa na kundi lao.
Mmoja wa wakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro, Bw. Oswald (kulia) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam sehemu ya msaada uliotolewa na wanafunzi hao.
Mmoja wa viongozi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo, Bi. Grace Minja (kulia) akimkabidhi mmoja wa watoto wa kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam sehemu ya msaada uliotolewa na wanafunzi hao.
Mmoja wa viongozi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo, Eng. Maeda akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 Sekondari ya Majengo akiwa na wanaye (kulia) akimkabidhi mtoto wa kituo cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam sehemu ya msaada uliotolewa na wanafunzi wenzake wahitimu.
Sehemu ya viongozi na wawakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro, wakipiga picha ya ukumbusho na watoto wa Kituo cha 'Hope Village For Orphans and Vulnerable Children' cha mkoani Kilimanjaro mara baada ya kukabidhi msaada katika kituo hicho.
Sehemu ya wawakilishi wa Kundi hilo mkoani mwanza wakipiga picha ya ukumbusho mara baadaa ya kukabidhi msaada katika kituo cha watoto yatima cha ‘Tanzania Childrens Rescue Centre (TCRC)’ jijini Mwanza.
Bw. Emmanuel Rimoy mwakilishi wa Kundi hilo mkoani Mwanza (wa pili kulia) akizungumza na watoto wa kituo cha watoto yatima cha ‘Tanzania Childrens Rescue Centre (TCRC)’ jijini Mwanza (hawapo pichani) mara baada ya kukabidhi msaada wao.
Sehemu ya msaada uliokabidhiwa Kituo cha 'Hope Village For Orphans and Vulnerable Children' cha mkoani Kilimanjaro na wawakilishi wa Kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo.
Sehemu ya msaada uliokabidhiwa na wawakilishi wa kundi mkoani Kilimanjaro Kituo cha 'Hope Village For Orphans and Vulnerable Children' cha mkoani Kilimanjaro.

KUNDI la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 katika Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro limetembelea vituo vitatu vya watoto wanaoishi katika maazingira maagumu na kutoa misaada mbalimbali ikiwa ni kuwafariji watoto hao.

Vituo vilivyonufaika na misaada hiyo ni pamoja na Kituo cha watoto yatima ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam, Kituo cha watoto yatima cha ‘Tanzania Childrens Rescue Centre (TCRC)’ jijini Mwanza na Kituo cha 'Hope Village For Orphans and Vulnerable Children' cha mkoani Kilimanjaro.

Akizungumzia msaada huo mmoja wa viongozi wa kundi hilo la wanafunzi waliohitimu Sekondari ya Majengo, Joachim Mushi alisema wanafunzi hao walichanga fedha kwa ajili ya kuwatembelea wahitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 4 tangu kuanzishwa kwa kundi hilo.

“…Wanakikundi waliamua kuchangishana fedha kwa ajili ya kuwatembelea wahitaji na kutoa chochote kwa lengo la kuwafariji yatima, na misaada kugawanywa katika mikoa mitatu yenye wawakilishi yaani Mwanza, Dar es Salaam na Mkoa wa Kilimanjaro…hii ni sehemu ya maadhimisho ya miaka minne ya kundi ambalo tulilianzisha 2014,” alisema Bw. Mushi.

Msaada uliyotolewa ni mifuko ya unga wa sembe, mchele, sukari, maharage, sabuni za kufulia na kuogea, mafuta ya kupikia, madaftari, vyombo vya kutumia pamoja na peni. 

Vingine ni pamoja na Dawa za meno, miswaki, biskuti, juisi, maji ya kunywa, mikate, majani ya chai, viatu pamoja na nguo mbalimbali za watoto vyote vikiwa na zaidi ya thamani ya zaidi ya milioni 1.8.
Eng. Willbard Gandu (aliyesimama) akizungumza na watoto wa kituo yatima cha ‘Green Pastures’ cha jijini Dar es Salaam kuwafariji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha watoto yatima ‘Green Pastures’, Mchungaji Douglas Kiseu (wa kwanza kulia) akiwatembeza wawakilishi katika kituo chake mara baada ya kukabidhi msaada wa kundi lao.
Picha ya pamoja ya wawakilishi wa Dar es Salaam wa kundi la Wasapu la Wanafunzi wahitimu kidato cha nne mwaka 2000 Sekondari ya Majengo iliyopo mkoani Kilimanjaro
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha watoto yatima ‘Green Pastures’, Mchungaji Douglas Kiseu akiwatembeza wawakilishi katika kituo chake kuangalia changamoto zilizopo katika kituo hicho. Pichani akiwaonesha tanki la kuhifadhia maji ya mvua ambalo kituo kimeshindwa kukifunika jambo amblo ni hatari kwa watoto kituoni hapo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad