Na Agness Francis, blogu ya Jamii
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amemuagiza mwanadada Amber Rutty anayejihusisha na masuala ya muziki wa bongo fleva nchini kufika katika kituo chochote cha Polisi hapa jijini leo kabla ya saa 12 Jioni.
Rc Makonda kupitia ukurasa wake wa Instagram ameweka picha ya mwanadada huyo na kuandika haya :
"Wakati TCRA wakijipanga kuchukua hatua, mimi namtaka mwenye picha hii kufika kituo chochote cha Polisi kilichopo karibu na eneo lake kabla ya saa 12 jioni. Na ukifika waambie umeitwa na RC Makonda watakupatia ujumbe wako" ameandika Makonda.
Hii inakuja baada kwa kosa la matumizi mabaya ya mtandao linalomkabili kwa kusambaza Video ya yenye maudhui ya kingono
na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuleta sintofahamu kubwa kwa Wanajaamii.
No comments:
Post a Comment