HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 11, 2018

KAMPUNI YATOA MAFUNZO WAFANYABISHARA WA VIFAA VYA UJENZI SOKO LA KARIAKOO

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya Imports International Tanzania imetoa mafunzo ya siku moja kuhusu jasi (gypsum) kwa wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi katika Soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Michuzi Blog leo jijini Dar es Salaam, Mtaalamu wa ujenzi wa kampuni hiyo  Stanley Katabarwa amesema lengo la kutoa mafunzo hayo ni wafanyabiashara ili wajue aina za gypsum kutokana na sehemu ambayo inakwenda kutumika.

Amesema wafanyabiashara wengi wanauza gypsum lakini hawajui matumizi sahihi, hivyo uwepo wao katika eneo hilo utasaidia wafanyabiashara hao kuuza gypsum kulingana na mahitaji ya mteja.

"Mara nyingi huwa tunakosea gypsum ya kutumia kulingana na shemu inayokwenda kutumia matokeo yake uimara ya hiyo sehemu inakuwa haipo.Tumeshafanya mafunzo ya aina mbili ambayo yalihusisha wadau wengine wa ujenzi na leo tunalenga mafundi na watu ambao wanauza, si kwamba wanauza bidhaa bila kuzielewa. Tunataka tu watu waelewe njia nzuri ya kutumia gypsum bora,"amesema.

Aidha Katabarwa amesema kampuni yao inazo gypsum za aina zote na hivyo kwa wanaohitaji wanaweza kufika katika ofisi zao ili wanunue na kuzitumia katika ujenzi.
 Mkaguzi wa wa Zimamoto Bandari, Dunstan Biyengo akitoa maelezo kwa wanafunzi wa chuo cha IFM waliofika katika maonesho ya maadhimisho ya miaka 13  ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari  ya Bandari  kuhusiana na kujihami na majanga yanayoweza kujitokeza wakati bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Nahodha wa Bandari, Kapten Nassor Mvuolana akiwapa maelezo wanafunzi wa chuo cha IFM waliofika katika maonesho ya maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari kuhusiana na kazi wanazozifanya wakati wa meli zinapoingia na zinapotoka  yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Afisa wa Bandari, Ernest Nyambo akizungumza na wanafunzi wa chuo cha IFM walipotembelea maonesho bandari ya Dar es Salaam katika ikiwa ni maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari  ambapo amewaeleza kuhusina  jinsi wanavypokea meli zinapoingia katika bandari hiyo maonesho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Wanafunzi wa IFM wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutembelea maonesho ya maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha IFM. Rayson Mbalamwezi akizungumza na waandishi habari kuhusiana na kushiriki na kujua vitu mbalimbali vinavyofanywa na banadari katika maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Masoko Mkuu wa TPA, Josephine Bujiku akizungumza na mwanafunzi kuhusiana na masoko wanavyoyapata kwa ndani ya nje ya nchi wakati maonesho ya bandari ikiwa  ni maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
 Meli ya Ngumi ikiwa imegeshwa kwa ajili ya maonesho ya bandari katika maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
Mfano wa meli iliyotengenezwa kwa ajili ya kutolea elimu ambayo imeletwa kwa ajili ya maonesho katika maadhimisho ya miaka 13 ya tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari yaliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad